Thursday, November 21, 2019



Kufuatia kuondoshwa kwa aliyekuwa Kocha Mkuu wa Yanga, Mwinyi Zahera ambaye hivi sasa yuko kwao Congo, inaelezwa kuwa mabosi wa timu hiyo wanataka kumpa timu Charles Boniface Mkwasa.

Taarifa hizo zimekuja ikiwa ligi bado ipo raundi ya kwanza ya msimu katika ligi, ikitajwa kuwa mabosi hao hawana mpango wa kusajili Kocha mpya kutoka nje ya nchi kwa kipindi hiki.

Maamuzi hayo yankuja Yanga wakiwa na nia ya kuwajenga vizuri wachezaji wake kisaikolojia na kutovuruga zaidi mwenendo wa timu hivyo badala yake wanataka kuendelea na Mkwasa kwa msimu huu.

Mkwasa alichukua nafasi hiyo na ameingoza Yanga kucheza mechi moja ya ligi huku akishinda kwa bao 1-0 ikiwa ni dhidi ya Ndada huko Mtwara.

Kuna uwekezekano Yanga ikaanza kusaka Kocha mwingine mara baada ya msimu kumalizika ambaye anaweza akatokea nchi za Afrika Magharibi ama nje kabisa ya bara la Afrika.

0 comments:

Post a Comment