Friday, December 29, 2017

Alexis Sanchez (kushoto) akishangilia na Laurent Koscielny baada ya kuifungia Arsenal mabao mawili dakika za 62 na 66 na kuiwezesha kushinda 3-2 dhidi ya wenyeji, Crystal Palace usiku wa jana Uwanja wa Selhurst Park mjini London. Bao lingine la Arsenal lilifungwa na Shkodran Mustafi dakika ya 25 wakati ya Palace yalifungwa na Andros Townsend dakika ya 49 na James Tomkins dakika ya 89

0 comments:

Post a Comment