Monday, September 7, 2020

Bingwa mara sita wa michuano ya US Open upande wa wanawake, Serena Williams amefanikiwa kutinga hatua ya 16 bora ya michuano ya hiyo kwa kumshinda Mmarekani mwenzake Sloane Stephens. Williams ambaye anashikilia nafasi ya tatu katika viwango vya vya ubora duniani,alishinda kwa alishinda kwa seti 2-6,6-2,,6-2. Ikumbukwe Serena anapigania kufikia rekodi ya kufikisha Grand Slam 24 kwa upande wa wanawake,atakipiga dhidi ya Maria Sakkari katika hatua ya 16 bora. Kwa upande mwingine mwanadada Victoria Azarenka alifuzu kwa kumshinda Iga Swiatek kwa seti kwa seti mbili za 6-4,na 6-2. Azarenka ambaye ni bingwa mara mbili wa US Open, atachuana na Karolina Muchova katika kusaka kucheza robo fainali.

0 comments:

Post a Comment