Tuesday, August 29, 2017

Ousmanne Dembele

Kandarasi hiyo ni ya pili kwa thamani baada ya ile ya hivi karibuni ya Neymar kuelekea PSG iliogharimu pauni milioni 200.
Dembele: Nafurahia sana kujiunga na Barca .
''Imekuwa ndoto yangu tangu nikiwa mdogo kuichezea Barca na sasa nimewasili''.
''Ndio klabu bora duniani ilio na wachezaji bora duniani''.
Mara ya mwisho kwa Dembele kuichezea Dortmund ni wakati wa kombe la Supercup mnamo tarehe 5 mwezi Agosti.
Klabu hiyo ya Bundesliga ilikataa ombi la Barca mapema mwezi Agosti , huku mchezaji huyo akiwa amepewa marufuku kwa kukosa mazoezi.

0 comments:

Post a Comment