Arsenal imekubali kumuuza mshambuliaji wake wa Kifaransa Olivier Giroud kwenda Chelsea kwa pauni milioni 18.
Kuondoka kwa Giroud kunafuatia ujio wa mshambuliaji wa kimataifa wa Gabon Pierre-Emerick Aubameyang anayetua Arsenal akitokea Borussia Dortmund kwa usajili unaovunja rekodi ya klabu - pauni milioni 55.5.
Giroud
aliichezea Arsenal mechi yake ya mwisho Jumanne usiku katika mchezo wa
Ligi Kuu ya England ulioshuhudia Arsenal ikilala 3-1.

0 comments:
Post a Comment