Kocha mpya wa Simba Patrick Aussems amesema falsafa yake katika timu zote alizofundisha ni kumiliki mpira na kutawala mchezo.
Anapenda kuona timu yake ikicheza soka la kuvutia kwa kupiga pasi.
Mashabiki wanaolipa viingilio na kukaa jukwaani kuangalia mechi wafurahi
na waondoke uwanjani wakiwa wameridhika. Hataki timu inayocheza soka la
‘butua-butua’.
“Falsafa yangu katika vilabu au timu za taifa nilizofundisha ni
kuhakikisha tunatawala mchezo, maana yeke timu yangu inatakiwa kumiliki
mpira ndio kitu muhimu kwangu”-Patrick Aussems.
“Nahitaji timu yenye mipango, tukiwa hatuna mpira kila mchezaji
anatakiwa kujua nini cha kufanya, tukishapata mpira wachezaji lazima
wajue wapi mpira unatakiwa kupelekwa.”
“Tunatakiwa kucheza mpira sio kubutua, huo ndio mpango wangu na wachezaji watatakiwa kufuata ili kuwapa burudani mashabiki.”
“Nahitaji kuona mashabiki wakifurahi baada ya kutoka uwanjani kutokana na timu yao kucheza vizuri na kutengeneza nafasi.”
“Sitaki kuona timu inapiga pasi mbili halafu inabutua mpira na hiyo
sio falsafa yangu. Wachezaji wanatakiwa kubadilika kutoka walivyokuwa
wanacheza misimu iliyopita. Lakini sipo hapa kukosoa makocha wengine
waliopita kwa sababu kila kocha alikuja na falsafa yake na mimi falsafa
yangu ni timu kucheza soka la kuvutia na ushindani ambalo litaridhisha
mashabiki wanaokuja uwanjani.”
“Bado sijakutana na wachezaji, jambo la kwanza kuwaeleza itakuwa ni
falsafa yangu. Nataka kuona kila mchezaji anafurahi wakati anacheza
uwanjani.”
Home
»
»Unlabelled
» Kocha mpya Simba hataki ‘butua-butua’
Saturday, July 21, 2018
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments:
Post a Comment