Kocha Emmanuel Amunike kupita kwa katibu Kidao amewaondoa wachezaji wa Simba SC Erasto Nyoni, Shomari Kapombe, Shiza Kichuya, Hassan Dilunga na Jonas Mkude kwa kushindwa kufika katika kambi ya Taifa Stars kwa muda waliopangiwa bila sababu za msingi.
Baada ya kuondolewa kwa wachezaji hao na kubakia Aishi Manula pekee aliyekubali kuwasili kambini kwa wakati na hatimae wasiofika nafasi zao zimezibwa na Salum Kimenya, Salum Kihimbwa, Paul Ngalema, David Mwantika, Frank Domayo na Kelvin Sabato.
0 comments:
Post a Comment