Mlinzi
aliyefanikiwa kuwakaba washambuliaji Heritier Makambo wa Yanga na
Meddie Kagere wa Simba, Kassian Ponela wa Mtibwa Sugar, amesema baada ya
kuwavaa nyota hao anaona Makambo ni bora zaidi.
Washambuliaji
hao kwa sasa ni gumzo kutokana na kuanza ligi kwa kasi kubwa, Kagere
ndiye kinara wa mabao Simba akiwa nayo matatu aliyofunga kwenye mechi
mbili na Makambo amefunga bao moja tu.
Ponela
amesema kuwa Makambo ambaye alifanikiwa kucheza naye kwenye mechi ya
ligi kuu msimu huu, ana nguvu na anajua kupambana na mabeki
ukilinganisha na Kagere pamoja na Emmanuel Okwi wanaocheza Simba.
Beki
huyo wa kati aliongeza kuwa alipata shida sana kumkaba Makambo
alipokutana naye na alijitahidi kumzuia asifunge lakini alishindwa
kutokana na uwezo mkubwa alionao mchezaji huyo.
“Kwangu mimi namuona Makambo kuwa ni bora zaidi,
nasema hivyo kwa sababu ana kila kitu anachotakiwa kuwa nacho
mshambuliaji, ana nguvu, kasi, uwezo wa kumiliki mpira, anajua kupiga
chenga lakini pia siyo muoga wa kupambana na mabeki wakorofi.
“Okwi
yeye ni mzuri, ana kasi na anajua kumiliki mpira lakini hana nguvu pia
ni muoga wakati Kagere yeye siyo muoga, ana nguvu, kasi na uwezo wa
kupambana lakini siyo mzuri sana katika kumiliki mpira na kupiga chenga,
kwa hiyo Makambo yupo vizuri,” alisema Ponela.

0 comments:
Post a Comment