Friday, December 20, 2019


HABARI ZA HIVI PUNDE
Arsenal imemteua kiungo wake wa zamani Mikel Arteta kuwa kocha mkuu wa klabu hiyo.
Kocha huyo mwenye miaka 37 ameshinda kombe la FA mara mbili akiwa na kikosi cha Gunners katika misimu mitano aliyokipiga na vigogo hao wa London.
Anachukua nafasi ya Mhispania mwenzake, Unai Emery ambaye alitimuliwa mwezi Novemba kutokana na matokeo mabovu.
Arteta anatokea Manchester City ambapo kwa miaka mitatu alikuwa kocha msaidizi wa Pep Guardiola.
"Tunahitaji kuwa tunagombea mataji makubwa," amesema Arteta.
"Suala hilo limebainishwa wazi katika mazugumzo yangu na (wamiliki wa Arsenal) Stan na Josh Kroenke na watu wengine waandamizi ndani ya klabu."
Arteta hata hivyo atachukua usukani rasmi siku ya Jumapili, akimuachia Freddie Ljungberg kuendelea kukaimu nafasi ya ukocha kwenye mchezo dhidi ya Everton kesho Jumamosi.
Arsenal kwa sasa wapo nafasi ya 10 kwenye msimamo wa Ligi ya Primia wakiwa na alama 22.

0 comments:

Post a Comment