Hakika ukizungumzia vilabu vyenye historia kubwa duniani
huwezi kuacha vilabu vya Liverpool au Manchester United kutokana na
ukongwe wao na historia ndani ya uwanja.
Sasa ukizungumzia klabu ya Liverpool imeingia katika rekodi mpya za
soka na ligi kuu ya Uingereza baada ya kushinda mechi yao ugenini dhidi
ya West Ham.
Liverpool imekuwa timu inayoongoza kwa kushinda mechi katika viwanja
vingi vya ugenini, yaani Liverpool imeshinda michezo katika viwanja
ambavyo sio vya kwao.
Majogoo hao wa London wamewahi kushinda katika viwanja 52 tofauti
katika ligi kuu ya Uingereza rekodi ambayo hakuna timu katika ligi hiyo
imeshawahi kushinda katika viwanja vingi kiasi hicho.
Wanaowafuatia Liverpool ni Manchester United na Arsenal ambao wote
wana rekodi sawa kwani hadi sasa timu hizo zimeshinda katika viwanja 50
tofauti.
Baada ya Manchester United na Arsenal wanaofuatia ni mabingwa wa ligi
kuu Uingereza klabu ya Chelsea ambao hadi sasa wameshinda katika
viwanja 48 tofauti.
Katika hali ya kustaajabisha klabu ya Aston Villa
ambayo hata haipo ligi kuu iko sawa na Manchester City na Tottenham
baada ya Aston Villa kushinda katika viwanja 46 sawa na vilabu hivyo
viwili ambavyo viko top four ya ligi kuu.
Home
»
»Unlabelled
» LIVERPOOL YAWEKA HISTORIA EPL
Tuesday, May 16, 2017
Subscribe to:
Post Comments (Atom)

0 comments:
Post a Comment