
Meneja wa Manchester City Pep
Guardiola amesema angekuwa amepigwa kalamu na klabu zake za hapo awali
za Barcelona na Bayern Munich kama angekamilisha msimu bila kupata
kikombe chochote.
City imeshindwa kupata ushindi tangu Guardiola
alipoanza kuiongoza mwanzo mwa msimu huu, na hawana uhakika kumaliza
katika nafasi nne bora katika ligi ya Premia licha ya kusalia na mechi
mbili.Upande wa Guardiola ulipoteza katika hatua ya timu 16 bora katika ligi ya klabu bingwa ulaya ,nusu fainali ya kombe la FA na kombe la ligi katika raundi ya nne.
"Katika hali yangu katika klabu kubwa , Ningefutwa. Ningetoka," Amesema mhispanio huyo.
0 comments:
Post a Comment