Wednesday, May 17, 2017


TOTAL AFCON U17 GABON2017MICHUANO ya kugombea Ubingwa wa Afrika kwa Vijana chini ya Miaka 17, TOTAL U-17 AFCON GABON 2017, iliyoanza Jumapili Leo itaendelea huko Nchini Gabon kwa Mechi 2 za Kundi A zitakazochezwa Stade de POG, Mjini Port Gentil.
Hapo Majuzi, katika Mechi za Kundi hilo Wenyeji Gabon walinyukwa 5-1 na Guinea wakati Ghana ikiichapa Cameroun 4-0.
Hii Leo, Guinea itacheza na Cameroun na Ghana kuivaa Gabon.
Hapo Kesho Alhamisi zitapigwa Mechi za Kundi B ambalo katika Mechi zao za kwanza matokeo yalikuwa Sare kwa Timu zote.
Juzi, Tanzania, maarufu kama Serengeti Boys, walitoka Sare 0-0 na Mali ambao ndio Mabingwa Watetezi.
Mechi hizo 2 za Kundi B zitachezwa Stade de L’Amitle, Mjini Libreville kwa Serengeti Boys kuanza na Angola na kufuatia Mali kucheza na Niger.
Washindi Wawili wa kila Kundi watatinga Nusu Fainali na Timu hizo 4 zitakazocheza Nusu Fainali ndizo hizo hizo zitafuzu kucheza Fainali za FIFA za Kombe la Dunia kwa Vijana U-17 huko Nchini India Mwezi Oktoba.
TOTAL U-17 AFCON GABON 2017
Ratiba/Matokeo:
**Saa za Bongo
***KUNDI A Mechi kuchezwa Mjini Port Gentil KUNDI B Mjini Libreville
MAKUNDI:
Jumapili Mei 14
KUNDI A
Gabon 1 Guinea 5
Cameroun 0 Ghana 4
Jumatatu Mei 15
KUNDI B
Mali 0 Tanzania 0
Angola 2 Niger 2
Jumatano Mei 17
KUNDI A
1730 Guinea v Cameroun [Stade de POG, Port Gentil]
2030 Ghana v Gabon [Stade de POG, Port Gentil]
Alhamisi Mei 18
KUNDI B
1730 Tanzania v Angola [Stade de L’Amitle, Libreville]
2030 Niger v Mali [Stade de L’Amitle, Libreville]
Jumamosi Mei 20
KUNDI A
2030 Gabon v Cameroun [Stade de POG, Port Gentil]
2030 Guinea v Ghana [Stade de L’Amitle, Libreville]
Jumapili Mei 21
KUNDI B
2030 Mali v Angola [Stade de L’Amitle, Libreville]
2030 Tanzania v Niger [Stade de POG, Port Gentil]
NUSU FAINALI:
Jumatano Mei 24
Stade de POG, Port Gentil
1730 Mshindi Kundi A v Mshindi wa Pili Kundi B
Stade de L’Amitle, Libreville
2030 Mshindi Kundi B v Mshindi wa Pili Kundi A
Jumapili Mei 28
Stade de L’Amitle, Libreville
1730 KUGOMBEA MSHINDI WA 3
2030 FAINALI

0 comments:

Post a Comment