Wednesday, June 28, 2017

 by alanus 

 Alvaro Morata
Mchakato wa Manchester United kumsajili mshambuliaji wa Real Madrid Alvaro Morata, 24, unasuasua baada ya Real kupandisha dau la mchezaji huyo hadi karibu pauni milioni 80 (Mirror).
Morata ambaye ameoa hivi karibuni, amelazimika kuondoka kwenye fungate yake ili kuharakisha uhamisho wake kwenda Old Trafford (AS).
Wasiwasi kuhusu hatma ya Cristiano Ronaldo unasababisha kuchelewa kutangazwa kwa uhamisho wa Alvaro Morata kutoka Real Madrid kwenda Manchester United (Diario Gol).
Tottenham wapo tayari kumpa mkataba mpya beki wake Toby Alderweireld, 28, ambaye ananyatiwa na Inter Milan (Daily Mirror).
Mshambuliaji wa Sunderland Jermain Defoe, 34, amekwama kwa sababu Bournemouth na West Ham zinachelea kumchukua kutokana na gharama kubwa za mchezaji huyo (Daily Star).

0 comments:

Post a Comment