Tuesday, November 21, 2017

Mwendeshaji baiskeli wa Rwanda Areruya Joseph ameshinda mashindano ya Tour of Rwanda.
Mwendeshaji baiskeli wa Rwanda Areruya Joseph ameshinda mashindano ya Tour of Rwanda.
Areruya Joseph, 21, anayechezea timu ya Dimension Data ya Afrika Kusini ameibuka mshindi wa mashindano ya kimataifa ya mbio za baiskeli maarufu Tour Of Rwanda yaliyomalizika jana mjini Kigali.
Mashindano hayo yalikuwa ya kuzunguka sehemu 7 tofauti za nchi hiyo, umbali wa kilomita 821.
Arerura Joseph amemshinda mpinzani wake wa karibu Mueritrea Eyob Metkel akimzidi kwa sekunde 28.
 
Mwendeshaji baiskeli wa Rwanda Areruya Joseph ameshinda mashindano ya Tour of Rwanda.
Image caption Mwendeshaji baiskeli wa Rwanda Areruya Joseph ameshinda mashindano ya Tour of Rwanda.
Wote wanachezea timu ya Dimension Data ya Afrika kusini.
Mashindano haya yalishirikisha waendeshaji baiskeli 73 kutoka timu 16 za mataifa mbali mbali duniani lakini wakamaliza waendesha baiskeli 43.

0 comments:

Post a Comment