MSHAMBULIAJI Neymar yuko shakani kuichezea Paris Saint-Germain katika mechi ya marudiano hatua ya 16 Bora Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Real Madrid baada ya Mbrazil huyo kuvunjika mfupa katika mguu wake na kumsababishia maumivu ya kifundo cha mguu.
Katika
ushindi wa PSG dhidi ya wapinzani wao, Marseille Jumapili, mwanasoka
huyo ghali zaidi duniani aliondoka uwanjani akibubujikwa machozi baada
ya kugongana na Bouna Sarr.
Amekwenda kufanyiwa vipimo baada ya mchezo huo walioshinda 3-0 Le Classique na vigogo wa Ligue 1 sasa wamethibitisha kwamba nyota huyo Mbrazil amumia kifundo cha mguu wake wa kulia.
Neymar yuko shakani kuichezea Paris Saint-Germain katika mechi dhidi ya Real Madrid baada ya kuumia 'enka' PICHA ZAIDI GONGA HAPA
Maumivu
hayo yanamaanisha Neymar sasa ataukosa mchezo huo wa marudiano wa PSG
iliyofungwa 3-1 kwenye mechi ya kwanza na kikosi cha Unai Emery
kitahitaji ushindi wa 2-0 kwenda Robo Fainali.
Vigogo hao wa Ufaransa pia wanahofia kumkosa bekji Mbrazil, Marquinhos baada ya naye kuelezwa pia ameumia.
Bahati
nzuri kwa PSG, mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 23 alihitaji siku
chache cha mapumziko na anatarajiwa kucheza mechi ya marudiano na
Madrid.
Pamoja
na kukabiliwa na majeruhi hao, PSG walidhihirisha ubora wao dhidi ya
mahasimu wao, Marseille Uwanja wa Parc des Princes Jumapili.
Kylian
Mbappe, Rolando na Edinson Cavani wote walifunga kikosi cha Emery
kikipaa kileleni kwa pointi 16 zaidi ya mahasimu wao, Marseille walio
nafasi ya tatu.
0 comments:
Post a Comment