Tuesday, July 16, 2019


Klabu ya Simba imesema kuwa msimu ujao watatumia jezi ya rangi nyekundu nyumbani na rangi nyeupe ugenini huku wakitumia rangi ya kijivu pale timu zinapogongana rangi.

Mtendaji mkuu wa timu ya Simba, Crecentius Magori amesema kuwa mpango huo ni kutokana na utaratibu wa Shirikisho la Soka la Afrika (Caf)

"Timu imeweka kambi nchini Afrika Kusini ikiwa ni maalumu kwa ajili ya maandalizi ya msimu ujao kwenye ligi pamoja na michuano ya kimataifa.

"Kuhusu jezi simba itatumia jezi nyekundu nyumbani, jezi Nyeupe ugenini na jezi za kijivu ambayo ni natural (halisi) kwa mazingira yeyote endapo timu zitakuwa zimevaa jezi zinazofanana," amesema.

0 comments:

Post a Comment