Tuesday, October 1, 2019

Arsenal players celebrate
Haki miliki ya picha Getty Images
Image caption Pierre-Emerick Aubameyang amekuwa mchezaji wa kwanza wa Arsenal kufunga magoli saba au zaidi katika mechi saba za mwazo za ligi tangu Dennis Bergkamp katika msimu wa 1997-98
Bundi yungali juu ya paa la kocha wa Manchester United, Ole Gunnar Solskjaer, hata baada ya kutoka sare katika mchezo wa jana usiku dhidi ya Arsenal.
Man United ikiwa nyumbani Old Trafford ilitangulia kupata goli kupitia shuti kali la kiungo Scott McTominay katika dakika ya 45.
Mshambuliaji Pierre-Emerick Aubameyang akawarudisha Arsenal mchezoni katika dakika ya 58, na mpaka dakika 90 zikikamilika matokeo yakasalia 1-1.
Arsenal wamerejea kwenye timu nne za kileleni kwenye jedwali la ligi kwa matokeo hayo, lakini kwa United sare hiyo haina unafuu wowote.
Bada ya kucheza mechi saba, United ipo katika nafasi ya 10, na alama 9 yakiwa ni matokeo mabaya zaidi katika miaka 30, kwa kushindwa walau kufikisha alama 10. Mara ya mwisho United kuwa na matokeo kama haya, 1989-90 walimaliza ligi katika nafasi ya 13.
Kwa mara ya kwanza toka mwaka 2000 Arsenal inanusurika kipigo katika dimba la Old Trafford katika mechi mbili mfululizo za ligi. Pia Arsenal imepiga mashuti mengi zaidi yaliyolenga lango (5) dhidi ya Man United (4) katika dimba hilo toka mwaka 2009.
Arsenal wana alama 12, Man United 9 jumla yao ni alama 21, sawa na alama za Liverpool ambao wapo kileleni.
Premier League table
Huu ulikuwa ni mchezo wa 28 ligi kwa Solskjaer kama kocha wa United, na kwa ujumla wake amekusanya alama 49, ikiwa ni alama mbili pungufu ya zile alizoshinda Jose Mourinho katika mechi zake 28 za mwisho.
Solskjaer, amesema, baada ya mchezo huo kuwa wana somo kubwa la kujifunza kutokana na matokeo hayo: "Mara ngapi tumekuwa tukiongoza 1-0 na tumeshindwa kufunga goli la pili? Tuna bonde refu la mambo ya kujifunza, na tutaendelea kufanya kazi kwa bidii, kwa uzoefu zaidi tutafanya maamuzi sahihi."

 Pierre-Emerick Aubameyang
"Hatukujituma ipasavyo mwanzoni mwa kipindi cha pili. Arsenal walijitoa kwa nguvu na kupata bao," amesema Solskjaer na kuongeza "Nilidhani tungeweza kupachika goli la pili mwishoni mwa mchezo, tulishambulia sana. Nimeshawahi kuwa katika hali kama hiyo nikiwa mchezaji, ambapo
Kwa upande wake kocha wa Arsenal Unai Emery amesema bado anataka matokeo bora zaidi kutoka kwa wachezaji wake: "Tuliingia uwanjani kushindana na tungeweza kufanya vyema zaidi. Tunaweza kumiliki mchezo zaidi na kutengeneza nafasi za kushinda. Tuna wachezaji wadogo ambao wanaweza kujiamini zaidi."

0 comments:

Post a Comment