Wednesday, October 30, 2019


Manchester United imekaribia kukamilisha uhamisho wa mshambuliaji wa Juventus na Croatia Mario Mandzukic 33 katika dirisha la uhamisho la mwezi Januari. (Tuttomercatoweb, via Express)
 
Arsenal, Liverpool na Manchester United wamekuwa wakiwasiliana na jopo la maafisa wa kiungo wa kati wa Uswizi na Borussia Dortmund Denis Zakaria, 22. (Sky Deutschland, via Inside Futbol)
Mshambuliaji wa Manchester City na Brazil Gabriel Jesus, 22, amepinga uvumi unaomuhusisha na Bayern Munich , akiandika katika mtandao wa Instagram kwamba uvumi huo ulikuwa uongo. (Manchester Evening News)
Gabriel Jesus aserma uvumi unaomuhusisha na klabu ya bayern ni wa uongo
Juventus iliwatuma maskauti kutazama mechi ya Liverpool dhidi ya Tottenham na walikuwa wakimuangazia mshambuliaji wa Liverpool na Misri Mohamed Salah, 27, mshambuliaji wa Tottenham na Korea Kusini Son Heung-min, 27, na kiungo wa kati wa Denmark Christian Eriksen, 27. (Tuttosport, via Mirror)
Newcastle iko tayari kumsaini kiungo wa kati mwenye urefu wa futi sita na nchi nne raia wa Ufaransa Ibrahima Sissoko, 21, kwa dau la ya £13m kutoka klabu ya ligi ya daraja la kwanza Strasbourg. (Sun)
Manchester United iko kifua mbele kumsaini Red Bull Salzburg na mshambuliaji wa Norway Erling Braut Halaand, 19. (Corriere dello Sport, via Manchester Evening News)
Mshambuliaji matata wa klabu ya Liverpool na Misri Mohammed Salah
Lyon imewasiliana na ajenti wa mshambuliaji Oliver Giroud kuhusu uhamisho wa mwezi januari kutoka Chelsea kwa raia huyo wa Ufaransa mwenye umri wa miaka 33 (Soccer Link, via Football.London)
Everton imekuwa ikimsaka kiungo wa kati wa Czech Republic na Spartak Moscow Alex Kral, 21. (Clubcall)
Mshambulauji wa Ubelgiji Eden Hazard, 28, amefichua kwamba alizungumza na rais wa Real Madrid Florentino Perezmwaka mzima kabla ya kupata uhamisho wa kuelekea Chelsea . (Talksport)
Wachezaji wa Arsenal wanamtaka kiungo wa kati wa Uswizi Granit Xhaka, 27, kusalia kuwa nahodha wa klabu hiyo licha ya kuwatukana mashabiki alipotoka katika mechi iliotoka sare ya 2-2 dhidi ya Crystal Palace siku ya Jumapili.. (Times, subscription required)
Nahodha wa klabu ya Arsenal Granit Xhaka
Leicester na Watford ni miongoni mwa klabu zinazomnyatia Ronald Sobowale – mpwa wa mchezaji wa Bayern Munich na nyota wa Austria David Alaba. Sobowale, 22, anaichezea timu ya daraja la nane katika ligi ya Bostick klabu ya kusini mashariki ya Whyteleafe na pia amefanyiwa majaribio na klabu ya Middlesbrough. (Mail)
Aliyekuwa mshambuliaji wa Manchester United na Sweden Zlatan Ibrahimovic, 38, amesema kwamba huenda akajiunga na klabu ya La Liga kufuatia huduma yake ya miezi kumi na nane akiichezea LA Galaxy. (Metro)
Kiungo wa kati wa zamani wa Tottenham Rafael van der Vaart amekiri kwamba alimwambia mwenyekiti wa Spurs Daniel Levy kumsaini kiungo wa kati wa Ajax na Morocco Hakim Ziyech, 26. (Star)
Kiungo hatari wa klabu ya Ajax na Morocco hakim ZiyeckHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Mshambuliaji wa Arsenal na England Stan Flaherty, 17, ametumia muda wake mwingi kufanyiwa majaribio katika klabu ya Newcastle mwezi huu . (Newcastle Chronicle)

0 comments:

Post a Comment