Jose
 Mourinho amekuwa kocha wa pili duniani katika mchezo wa soka kulipwa 
fedha nyingi zaidi baada ya kuanguka saini ndani ya klabu ya Tottenham 
ambayo itakuwa inampatia kiasi cha pauni milioni 15 kwa mwaka.

Kusaini kwake tu, kwa miamba hiyo ya soka ya Kaskazini mwa jiji la London, Mourinho atakuwa anapokea kitita cha fedha mara mbili ya mshahara ambao alikuwa akilipwa kocha aliyetimuliwa kazi, Mauricio Pochettino.
Hii
 ni kwa mara ya kwanza katika historia ya klabu ya Tottenham, kumwajiri 
kocha mwenye kariba ya Mourinho ambaye tayari ameshinda mataji 25 kwenye
 taaluma hiyo huku wakitoa kitita kinono.

Mourinho
 sasa atakuwa akipokea mshara wa Pauni Milioni 15 kwa mwaka kiasi 
ambacho kinamfanya kushika nafasi ya pili (2), kwa malipo ambayo wanapa 
makocha wanaofundisha mchezo wa soka.
Mreno
 huyo anakuwa nyuma ya Pep Guardiola ambaye anashika nafasi ya kwanza 
akipokea Pauni Milioni 20 baada ya kuongeza mkataba wake ndani ya 
Manchester City msimu uliyopita 2018 ambao atashuhudiwa akiwa hapo kwa 
miaka mingine miwili.
Mhispania huyo 
ndiyo kinara kwa makocha wote wa soka duniani akipokea kiasi hicho cha 
pesa pauni milioni 20 kwa mwaka na akidhihirisha uhalali wa yeye kupokea
 mkwanja huo baada ya kuchukua ubingwa wa Premier League ‘back-to-back’.
0 comments:
Post a Comment