Wednesday, February 5, 2020


Kocha wa klabu ya Polisi Tanzania, Malale Hamsini amesema kuwa mchezo wao dhidi ya Simba SC ulikuwa mzuri na wenye ufundi zaidi, lakini mwisho wa yote wanamuachia Mungu kwa kuwa ndiyo aliyopanga matokeo yao kuwa hivyo.

”Bila shaka, tumejionea leo wote ‘game’ ilikuwa nzuri na yenye ufundi zaidi. Lakini mwisho wa yote tunamuachia Mwenyezi Mungu ndiye aliyepanga matokeo yawe hivi.” Kauli ya kocha wa Polisi Tanzania, Malale Hamsini akizungumza na waandishi wa habari Uwanja wa Taifa baada ya kumalizika kwa mchezo huo.
Malale Hamsini akijibu maswali ya waandishi ameongeza kuwa ”Ni kweli tulitakiwa kumaliza ‘game’ mapema lakini kilichotushinda ni uzoefu tu, lakini mechi ilikuwa nzuri na vijana wangu walijituma zaidi.”
”Chumba chetu kilizimwa umeme, sasa hatujui nini tatizo.” Alimazima Kocha wa Polisi Tanzania, Malale Hamsini ambaye alichukua nafasi ya Seleman Matola aliyetimkia Simba SC.
Kwenye mchezo huo Polisi Tanzania ilijikuta ikipoteza kwa kipigo cha magoli 2 – 1 mbele ya Mnyama mkali Simba.
Image result for Je, goli la kwanza la Simba dhidi ya Polisi Tanzania ni off side? Tazama uchambuzi hapa"
Hata hivyo mechi hiyo imegubikwa na lawama kutoka kwa mashabiki na baadhi ya wachambuzi wa soka nchini wakidai bao la kwanza la Simba SC lilikuwa ‘offside’ kutoka kwa John Bocco.

0 comments:

Post a Comment