Thursday, April 16, 2020

winga
Winga wa kimataifa wa Ujerumani na Manchester City Leroy Sane, 24, anakaribia kuhamia Bayern Munich kwa kiasi cha £70m.(Mirror)
Klabu za Ligi ya Premia zitakutana Ijumaa kujadili uwezekano wa msimu huu kumalizika Juni 30. Ikiwa uamuzi huo utaamuliwa kwa kura, basi klabu 14 kati 20 zitahitajika kukubaliana. (Guardian)
Kiungo wa kati wa Bayer Leverkusen na Ujerumani Kai Havertz, 20, amedokeza kuwa yuko tayari kuhamia ughaibuni, huku Liverpool ikiwa ni miongoni mwa klabu ya Ligi ya Primia inayomtaka. (Sport Bild - in German)
Mshambuliaji wa Chelsea na Ufaransa Olivier Giroud
Mshambuliaji wa Chelsea na Ufaransa Olivier Giroud, 33, yuko tayari kupunguziwa mshahara ili apate fursa ya kuhamia Inter Milan msimu huu. (Gazzetta dello Sport - in Italian)
Beki wa Manchester United na Argentina Marcos Rojo, 30, anataka kurefusha mkataba wake wa sasa wa mkopo nyumbani kwa Estudiantes kwa sababu amecheza mara moja tu na kujeruhiwa kabla ya ligi kusitishwa katokana na mlipuko wa vurusi vya corona. (Manchester Evening News)
Adam Lallana
Mabingwa wa Italia, AC Milan wameamua kuwasilisha ofa ya kumnunua kiungo wa kati wa England Adam Lallana msimu huu. Mkataba wa mchezaji huyo wa zamani wa Southampton, 31, katika klabu ya Liverpool unamalizika mwisho wa Juni. (Mirror)
Arsenal inatarajiwa kamuuza mshambuliaji wa Ufaransa Alexandre Lacazette mwisho wa msimu, huku Atletico Madrid wakipigiwa upato kumnunua kiungo huyo wa miaka 28. (AS - in Spanish)
Arsenal wanakaribia kukamilisha uhamisho wa bure wa beki wa Ufaransa wa miaka 27 Layvin Kurzawa kutoka Paris St-Germain.(Daily Star)
Zinedine Zidane
Arsenal huenda ikampoteza mshambuliaji wa Gabon Pierre-Emerick Aubameyang, ambaye anatakiwa na Real Madrid. Kiungo huyo wa miaka 30-anatakiwa Zinedine Zidane kuchukua nafasi mbadala ya ya mshambuliaji wa Inter Milan Lautaro Martinez - ambaye anataka kuhama klabu hiyo ya Italia kuenda Barcelona.(Sport - in Spanish)
Beki wa Leicester wa Austria Christian Fuchs
Beki wa Leicester wa Austria Christian Fuchs, 34, bado hajakata shauri ikiwa atarefusha mkataba wake katika uwanja wa King Power ama ahamie Marekani kujiunga na familia yake. (Daily Mail)
Kipa wa Liverpool Loris Karius amesema bado anawasiliana na Jurgen Klopp, japo yuko klabu ya Uturuki ya Besiktas, hana uhakika kuhusu hatima yake ya baadae. Mkataba wa Mjerumani huyo wa miaka, 26, Anfield unaendelea hadi 2022. (Sky Sports)

0 comments:

Post a Comment