details mei 30 2017

Barcelona wamemteua Ernesto Valverde
kuwa mkufunzi wao mkuu kwa mkataba wa miaka miwili, ambapo anaweza
akaongezewa mwaka mwingine wa tatu.
Valverde ni mshambuliaji wa
zamani wa Barca na alitangaza wiki iliyopita kwamba angeacha kazi
Athletic Bilbao baada ya kuwaongoza kwa miaka minne.Anachukua nafasi ya Luis Enrique aliyetangaza Machi kwamba angeihama klabu hiyo iliyomaliza nafasi ya pili La Liga msimu huu.
Anaondoka baada ya kumaliza mkataba wake wa miaka mitatu
0 comments:
Post a Comment