mei 29 2017

Manchester City wanakaribia kumnunua kipa wa mabingwa wa ligi ya Ureno Benfica Ederson Moraes kwa jumla ya £33m.
Meneja
wa City Pep Guardiola amekuwa akimtafuta mchezaji huyo wa Brazil kwa
muda na sasa amepata nafasi baada ya kumwachilia kipa wa klabu hiyo
Willy Caballero Ijumaa.Baada ya ushindi wa 2-1 katika fainali ya Kombe la Ligi nchini Ureno, Moraes alisema kuna uwezekano hiyo ikawa ilikwua mechi yake ya mwisho kuwachezea benfica.
Taarifa zinasema Guardiola pia anataka kumnunua beki wa kati Mfaransa anayechezea Monaco Benjamin Mendy, 22.
Baada ya kukosa kushinda kikombe chochote msimu wake wa kwanza kama meneja City, Guardiol amepanga kufanyia mabadiliko makubwa kikosi cha klabu hiyo kabla ya msimu ujao kuanza.
0 comments:
Post a Comment