Monday, May 29, 2017



CHELSEA-TUZOKIUNGO wa Chelsea Eden Hazard ameteuliwa kuwa ndie Mchezaji Bora wa Mwaka na N'Golo Kante kutwaa Tuzo ya 'Mchezaji wa Wachezaji' katika Hafla maalum ya kugawa Tuzo za Mabingwa Wapya wa England Chelsea zilizofanyika Jana Usiku Jijini London.
Mbali ya Tuzo ya Mchezaji Bora wa Mabingwa hao, pia Hazard alizoa Tuzo ya Goli Bora la Msimu kwa Goli lake alilofunga Februari 4 kwa juhudi binafsi dhidi ya Arsenal.
Pia, Kepteni wa Chelsea, John Terry, ambae ndie anastaafu hivi sasa baada kuitumikia Chelsea kwa Miaka 22, amepewa Tuzo maalum kwa Utumishi wake.
Meneja wa Mabingwa hao Antonio Conte ndie aliekabidhi Tuzo hizo ambazo Washindi wake walipatikana kwa Kura za Washabiki.
Mbali ya Mshindi Hazard, Wagombea wengine wa Tuzo ya Mchezaji Bora walikuwa Cesar Azpilicueta, David Luiz na Kante.
CHELSEA - Washindi wa Tuzo:
GOLI LA MSIMU: Eden Hazard
MCHEZAJI WA WACHEZAJI: N'Golo Kante
MCHEZAJI BORA KINAMAMA: Karen Carney
MCHEZAJI BORA CHUONI: Mason Mount
MCHEZAJI BORA WA MWAKA: Eden Hazard
TUZO MAALUM: John Terry

0 comments:

Post a Comment