- Created: Monday, 29 May 2017 08:23
Mbali ya Tuzo ya Mchezaji Bora wa Mabingwa hao, pia Hazard alizoa
Tuzo ya Goli Bora la Msimu kwa Goli lake alilofunga Februari 4 kwa
juhudi binafsi dhidi ya Arsenal.
Pia, Kepteni wa Chelsea, John Terry, ambae ndie anastaafu hivi sasa
baada kuitumikia Chelsea kwa Miaka 22, amepewa Tuzo maalum kwa Utumishi
wake.
Meneja wa Mabingwa hao Antonio Conte ndie aliekabidhi Tuzo hizo ambazo Washindi wake walipatikana kwa Kura za Washabiki.
Mbali ya Mshindi Hazard, Wagombea wengine wa Tuzo ya Mchezaji Bora walikuwa Cesar Azpilicueta, David Luiz na Kante.
CHELSEA - Washindi wa Tuzo:
GOLI LA MSIMU: Eden Hazard
MCHEZAJI WA WACHEZAJI: N'Golo Kante
MCHEZAJI BORA KINAMAMA: Karen Carney
MCHEZAJI BORA CHUONI: Mason Mount
MCHEZAJI BORA WA MWAKA: Eden Hazard
TUZO MAALUM: John Terry
MCHEZAJI WA WACHEZAJI: N'Golo Kante
MCHEZAJI BORA KINAMAMA: Karen Carney
MCHEZAJI BORA CHUONI: Mason Mount
MCHEZAJI BORA WA MWAKA: Eden Hazard
TUZO MAALUM: John Terry
0 comments:
Post a Comment