COPA DEL REY: MESSI, NEYMAR, ALCACER WAIPA KOMBE BARCA!
- Details
- Created: Sunday, 28 May 2017 08:29
Hii ni mara ya 3 mfululizo kwa Barca kutwaa Kombe hili.
Fainali hii ilichezwa huko Vicente Calderon Jijini
Madrid na ndio Mechi ya mwisho kabisa kwa Kocha wa Barca Luis Enrique
ambae anaondoka Klabuni hapo.
Bao zote za Mechi hiyo zilifungwa Kipindi cha Kwanza.
Barca walitangulia kufunga Dakika ya 30 kupitia Lionel Messi na Alaves kusawazisha kwa Frikiki ya Theo Hernandez Dakika ya 33.
Barca walipiga Bao 2 za chapchap Dakika za 45 na 48 kupitia Neymar na Alcarer na kwenda Haftaimu 3-1 mbele.
0 comments:
Post a Comment