Thursday, July 13, 2017

By alanus

 QUerrey alikuwa katika kiwango bora kwenye mchezo huo
Bingwa mtetezi wa michuano ya Wimbledon Andy Murray amesukumwa nje ya mashindano hayo na Sam Querrey katika hatua ya nusu fainali.Murray ambaye amekuwa na majeraha hakuweza kucheza vizuri katika mpambano huo.
Querrey, 29, ameshinda kwa seti 3-6 6-4 6-7 (4-7) 6-1 6-1 na kuwa Mmarekani wa kwanza kufanya hivyo tokea Andy Roddick alipofika katika hatua hiyo mwaka 2009.
Muray hakua katika hali nzuri katika hatua za mwisho za mpambano dhidi ya QUerrey
Murray, 30, aliongoza awali lakini maumivu ya goti yalimfanya ashindwe kuuhimili mchezo.
Majeraha aliyoyapata pia Novak Djokovic yanamfanya Murray aendelee kushikilia namba moja.
Djokovic namba mbili kwa ubora duniani, alipaswa kushinda mchezo dhidi ya Tomas Berdych lakini majeraha ya kiwiko yakakatisha matumaini hayo.

0 comments:

Post a Comment