Tuesday, September 26, 2017

Kocha wa West Brom, Tony Pulis jana alimuanzisha Gareth Barry dhidi ya Arsenal akaweka rekodi ya kucheza mechi nyingi zaidi Ligi Kuu ya England PICHA ZAIDI GONGA HAPA  


WALIOCHEZA MECHI NYINGI ZAIDI LIGI KUU ENGLAND KIHISTORIA 

Gareth Barry - 633
Ryan Giggs - 632
Frank Lampard - 609
David James - 572
Gary Speed - 535
Emile Heskey - 516
Mark Schwarzer - 514
Jamie Carragher - 508
Phil Neville - 505
Rio Ferdinand - 504
Steven Gerrard - 504
KIUNGO wa West Bromwich Albion, Gareth Barry jana amevunja rekodi ya nyota wa zamani wa Manchester United, Ryan Giggs kucheza mechi nyingi katika Ligi Kuu ya England.
Barry amesema wanawe wamelazimika kutokwenda shule ili waende kumshuhudia akicheza mechi ya kuvunja rekodi usiku wa jana dhidi ya Arsenal Uwanja wa Emirates. 
Barry, mwenye umri wa miaka 36 sasa, jana amecheza ya 633 ya Ligi Kuu England baada ya kuanzishwa kwenye mechi dhidi ya The Gunners.
Mchezaji huyo wa zamani wa Aston Villa, Manchester City na Everton anavunja rekodi ya gwiji wa Wales, Giggs ambaye alicheza mechi 672 akiwa na Manchester United.  
Kocha wa Arsenal, Arsene Wenger alimzawadia Barry jezi iliyosainiwa namba 633 na klabu hiyo ikatweet baada ya mechi: "Hongera Gareth Barry kwa kucheza mechi ta rekodi katika Ligi Kuu ya England, (pongezi) kutoka kwetu sote wa Arsenal,"

0 comments:

Post a Comment