Monday, September 18, 2017


UTD INAWATAKA SAUL & NAINGGOLAN


Nainggolan Roma
Manchester United wamepania kuwasajili Saul Niguez na Radja Nainggolan kuziba nafasi ya Michael Carrick, kwa mujibu wa  Daily Star .
Mashetani Wekundu walituma skauti katika mechi ambao Roma walitoa sare dhidi ya Atletico Madrid kwenye Ligi ya Mabingwa wiki iliyopita kuangalia viungo hao wawili.
Carrick, 36, anatarajiwa kuondoka Old Trafford mwishoni mwa kampeni za msimu huu.

SPURS YAMFUKUZIA GOMES


Andre Gomes Granada Barcelona La Liga
Tottenham wanatamani kumsajili kiungo mahiri wa Barcelona Andre Gomes na kumleta kwenye Ligi Kuu Uingereza, kwa mujibu wa  the Sun .

BARCA SASA YAMGEUKIA MANE


Sadio Mane Liverpool
Baada ya kumkosa Philippe Coutinho, Barcelona sasa wanamfuatilia kwa karibu sana mshambuliaji wa Liverpool Sadio Mane, kwa mujibu wa Mirror .
Miamba hao wa Catalan walishuhudia ofa zao nyingi zikikataliwa kwa ajili ya mchezaji huyo wa kimataifa wa Brazili lakini bado watajaribu kwa mchezaji mwingine wa Anfield.

MAN CITY YAPANGA KUZUNGUMZA NA DE BRUYNE


Kevin De Bruyne, Man City
Manchester City wapo tayari kumtunuku mkataba mpya Kevin De Bruyne wenye thamani ya paundi 200,000 kwa wiki baada ya kiwango safi, limeripoti Mirror .
Mkataba wa Mbelgiji huyo umebakisha miaka mitatu kumalizika, lakini Pep Guardiola anatamani kumpa mkataba mwingine mpya ili kumfunga zaidi.

MAN UTD YAMFUKUZIA ZIVKOVIC


Andrija Zivkovic Ruca Chaves Benfica Tondela 01222017
Manchester United wamemwongeza winga wa Benfica Andrija Zivkovic katika orodha ya wachezaji wanaotaka kuwasajili, kwa mujibu wa  O Jogo .
Mashetani Wekundu walituma skauti kumfuatilia Mserbia huyo katika mechi za katikati ya juma za Ligi ya Mabingwa.

LEWANDOWSKI ANATAKA KUONDOKA BAYERN


Robert Lewandowski Bayern Munich Bundesliga 08262017
Mshambuliaji wa Bayern Munich Robert Lewandowski amemtaka wakala wake kumtafutia timu mpya uhamisho wa majira ya joto 2018, kwa mujibu wa  AS .
Klabu nyingi zinamtaka mchezaji huyo wa kimataifa wa Polandi, lakini kwa mujibu wa habari anapendelea kujiunga na klabu ya Real Madrid.

MULLER ANAPENDELEA KWENDA MAN UTD


Thomas Muller Carlo Ancelotti Bayern Munich 18072017
Thomas Muller angependa kujiunga na Manchester United, ikiwa ataondoka Bayern Munich kutua Ligi ya Uingereza, kwa mujibu wa The Sun .
Mchezaji huyo wa kimataifa wa Ujerumani amekuwa na wakati mgumu Bayern na alitajwa kwenye tetesi za Arsenal, Chelsea na Liverpool majira ya joto.

CHELSEA YAMTUPIA JICHO CHIELLINI


Giorgio Chiellini Juventus
Beki wa Juventus Giorgio Chiellini bado jaanza mazungumzo ya mkataba mpya na klabu yake, kwa mujibu wa Calciomercato.com .
Mkataba wa Chiellini unaisha mwisho wa msimu huu na kwa mujibu wa habari Chelsea wanaifukuzia saini yake, kwa hiyo ni habari njema kwa kocha wa zamani wa Juve, Antonio Conte.

BARCA HAWATAMRUDIA COUTINHO UHAMISHO WA JANUARI


HD Coutinho
Barcelona hawatarudi na ofa mpya kumsajili kiungo wa Liverpool Philippe Coutinho dirisha la uhamisho Januari, kwa mujibu wa Marca 

MAN UTD YAMFUKUZIA WINGA WA ROMA


Mirko Antonucci, Roma, 2017
Manchester United wanajipanga kumsajili kinda wa Roma Mirko Antonucci, ambaye hajawahi kufanya mkataba rasmi kama mchezaji mkubwa, kwa mujibu wa TransferMarketWe b.

ATLETICO YAKARIBIA KUMNASA COSTA


Diego Costa Chelsea Premier League
Atletico Madrid wana tumaini la kukamilisha usajili wa nyota wa Chelsea anayetaka kuondoka Stamford Bridge, mshambuliaji Diego Costa, kwa mujibu wa  Marca .
Ripoti zinadai kuwa klabu mbili hizo zipo kwenye mazungumzo kwani Costa sasa yupo tayari kurudi Ulaya baada ya kugomea Brazili.

ARSENAL BADO INAMFUATILIA JANKTO


Jakub Jankto Udinese Serie A
Arsenal bado inaendelea kumfuatilia kiungo wa Udinese Jakub Jankto, kwa mujibu wa  Calciomercato.com .
AC Milan na Juventus pia zimeonesha nia ya kutaka kumsajli Jankto, ambaye ameweka bayana shauku yake kucheza Ligi Kuu Uingereza.

BARCA KUMTOLEA OFA MPYA SERI


Jean Michael Seri Nice
Barcelona wanajipanga kutoa ofa mpya kwa ajili ya kiungo wa Nice Jean-Michael Seri katika dirisha la uhamisho la Januari, kwa mujibu wa  Sport .
Seri alivunjika moyo Barcelona waliposhindwa kukamilisha usajili wa mchezaji huyo kwa euro milioni 40 zilizokuwa zikihitajika majira ya joto, lakini sasa klabu hiyo ya Catalan imeamsha upya nia yao kumsajili mchezaji huyo wa kimataifa wa Ivory Coast.

MAN UTD KUTOA £100M KWA AJILI YA GRIEZMANN


Antoine Griezmann France 2017
Manchester United wapo tayari kutoa kitita cha paundi milioni 100 kumsajili mshambuliaji wa Atletico Madrid Antoine Griezmann mwaka ujao, kwa mujibu wa  Daily Star .
Mchezaji huyo wa kimataifa wa Ufaransa amehusishwa vikali na tetesi za kutaka kutua Old Trafford, lakini kufungiwa kwa klabu yake kufanya usajili kulimfanya aendelee kubaki Hispania.

MAN CITY YASAINI NYOTA KINDA WA U.S.


Erik Palmer-Brown MLS Homegrown Game
Beki wa kati wa Sporting Kansas City Erik Palmer-Brown atajiunga na Manchester City kwa mujibu wa  Metro na  Kansas City Star .
Kinda huyo wa Marekani ataondoka MLS mara mkataba wake utakapokwisha mwishoni mwa 2017, baada ya kusaini mkataba wa miaka minne na timu hiyo ya Pep Guardiola.

STERLING BADO YUMO KWENYE RADA ZA ARSENAL


Raheem Sterling, Man City
Winga wa Manchester City Raheem Sterling bado ni shabaha ya washindani wa Ligi Kuu Uingereza, Arsenal kwa mujibu wa Daily Mail.
Mchezaji huyo wa zamani wa Liverpool ambaye yupo tayari kutua London, aliripotiwa kutakiwa na Gunners kama sehemu ya dili la Alexis Sanchez.

PEP ACHAGUA BEKI MPYA WA KATI


Toby Alderweireld Tottenham
Kocha wa Manchester City Pep Guardiola anatarajia kusaini beki wa Tottenham, Toby Alderweireld kama mrithi wa Vincent Kompany, kwa mujibu wa The Sun .
Wakala wa mchezaji huyo amedai kuwa beki huyo hana furaha kulingana na kile anacholipwa White Hart Lane, £50,000 kwa wiki kwa mujibu wa ripoti.

COSTA KUHAMIA MADRID


Diego Costa Chelsea
Diego Costa anayetaka kuondoka Chelsea ameihamishia familia yake Madrid katika jitihada zake kushinikiza kutua Atletico Madrid, kwa mujibu  wa   The Sun .

COUTINHO AUMIZWA NA DILI LA BARCA LILILOSHINDIKANA


Phil Coutinho
Mshambuliaji wa Liverpool Philippe Coutinho amebaki na jeraha la moyo kufuatia mipango yake kwenda Barcelona kukwama majira ya joto, kwa mujibu wa Don Ballon .
Mchezaji huyo wa kimataifa wa Brazili anahisi miamba hao wa Catalan walihitaji kufanya jitihada zaidi kwa ajili ya saini yake. Habari zinadai kuwa alipewa uhakika na uongozi wa Barca kuwa watamsajili lakini mambo yakawa kinyume.

LIVERPOOL YAPATA USHINDANI KWA VAN DIJK


Virgil van Dijk Southampton
Juventus itafanya mchakato wa kumsajili beki wa kati wa Southampton Virgil van Dijk dirisha la uhamisho wa majira ya baridi litakapofunguliwa Januari, kwa mujibu wa   the Mirror .

ARSENAL YAKUBALI KUMSAJILI LEMAR


Thomas Lemar Monaco
Arsenal wamekubali masharti ya kumsajili Thomas Lemar wa Monaco uhamisho wa Januari. Watatumia Euro milioni 100 kwa ajili ya mchezaji huyo wa Monaco, ambaye atalipwa paundi 250,000 kwa wiki, kwa mujibu wa  The Star .

MADRID YAMFUATILIA MSHAMBULIAJI WA LEIPZIG


Timo Werner RB Leipzig
Real Madrid wameonesha nia ya kumsajili mshambuliaji wa RB Leipzig Timo Werner wanapotafuta mbinu za kuimarisha safu yao ya mashambulizi, kwa mujibu wa Jugones, via AS.

MOURINHO KUSAINI MKATABA MPYA MAN UNITED


Jose Mourinho
Jose Mourinho yu mbioni kupewa mkataba mpya Manchester United kufuatia mwanzo mzuri wa msimu wa Ligi Kuu Uingereza, kwa mujibu wa habari kutoka  Telegraph .

0 comments:

Post a Comment