Usiku huu kulikuwa na mechi za mwisho kwa wiki hii za
kirafiki kabla ya kurejea katika mechi za vilabu, na timu kubwa za
mataifa mbali mbali zilikuwa uwanjani.

Romelu
Lukaku ameendelea kufunga na sasa katika mechi mbili za timu ya taifa
kwa wiki hii anakuwa amefunga mabao 3 na sasa anakuwa mfungaji bora wa
Ubelgiji wa muda wote, ana mabao 31 jumla.

Katika
mechi nyingine Mabao mawili ya Alexandre Lacazette yaliibeba Ufaransa
na kuwapa sare ya mbili mbili dhidi ya mabingwa wa dunia timu ya taifa
ya Ujerumani ambao mabao yao yaliwekwa kimiani na Timo Werner pamoja na
Sandro Wagner.
Uholanzi walifanikiwa kuipiga Romania kwa mabao 3 kwa nunge huku
mabao ya Uholanzi yakiwekwa kimiani na Memphis Depay, Ryan Babel pamoja
na lile la Luuk De Jong.

Timu
ya taifa ya Hispania ililazimishwa suluhu ya tatu tatu na waandaaji wa
kombe la dunia Urusi huku mabao ya Hispania yakiwekwa kimiani na Jordi
Alba na Sergio Ramos (2) na ya Urusi yakifungwa na Fedor Smolov(2) na
Alexey Miranchuk.

Nigeria
waliishangaza Argentina kwa kutoka nyuma ya bao 2 wakasawazisha na
kisha kuibuka kidedea kwa ushindi wa bao 4 kwa 2, Alex Iwobi(2),Kelechi
Iheanacho na Brian Idowu walikuwa mashujaa wa Nigeria huku Ever Banega
na Sergio Aguero wakiifungia Argentina.

Pale
Wembley kulikuwa na mchezo wa kukata na shoka ambapo Brazil walikuwa
wageni wa Uingereza katika mchezo ulioisha kwa sare ya bila kufungana.
0 comments:
Post a Comment