
WAKATI
timu ikijiandaa na mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara dhidi ya Ruvu Shooting
kutoka Pwani, utakaopigwa Jumapili kwenye Uwanja wa Taifa, Kocha Msaidizi wa
Simba, Masoud Djuma, amesema wanahitaji kupata ushindi ili kuwaongezea ari
wachezaji wao kuelekea mchezo wa Kombe la Shirikisho Afrika.
Akizungumza
na gazeti la Nipashe jana jijini Dar es Salaam, Djuma, ambaye timu yao
inadhaminiwa na Kampuni ya Kubashiri Matokeo Michezoni ya SportPesa, alisema
kuwa timu inayoshinda inakuwa imara katika mchezo unaofuata na uwezo wa
kujiamini wa wachezaji wake unaongezeka.
Djuma
alisema wanaendelea na mazoezi kila siku kwa sababu wanataka kuona wanapata
pointi tatu katika kila mchezo wanaocheza hatua ya lala salama ambayo bingwa wa
Ligi Kuu Bara hupatikana.
"Tunajua
tuko mbele na wenzetu wanatuangalia ili watufikie, tumejipanga kuwakimbia na
hili litafanikiwa kwa sisi kuendelea kushinda, kufanya vizuri kwenye ligi ya
Tanzania, kutatuweka vizuri pia kwenye mashindano ya CAF (Kombe la Shirikisho
Afrika)," alisema kocha huyo raia wa Burundi.
Katika
hatua nyingine, Mkuu wa Idara ya Mawasiliano wa Shirikisho la Soka Tanzania
(TFF), Clifford Ndimbo, alisema jana kuwa mchezo kati ya Simba na Azam FC
unaotarajiwa kufanyika Februari 7, mwaka huu, utafanyika kama ulivyopangwa na
ule wa ugenini dhidi ya Mwadui FC umesogezwa mbele.
Baada ya
mchezo dhidi ya mabingwa wa Kombe la Mapinduzi, vinara hao wa Ligi Kuu Tanzania
Bara watajiandaa kuwakaribisha Gendarmarie Nationale katika mchezo wa kwanza wa
raundi ya awali ya mashindano ya kimataifa ya Kombe la Shirikisho.
Simba ndio
vinara wa ligi wakiwa wamejikusanyia pointi 35 na ni timu pekee ambayo
haijafungwa katika mechi za mzunguko wa kwanza wakifuatiwa na Azam FC wenye
pointi 30, mabingwa watetezi, Yanga wao wana pointi 28 na Singida United yenye
pointi 27 wako katika nafasi ya nne kwenye msimamo.
Wekundu wa
Msimbazi watashuka uwanjani pia wakiwa na kumbukumbu ya ushindi katika mechi
zake nne zilizopita ambazo ilipata pointi 12 na mabao 12 ya kufunga huku pia
wakikumbuka kichapo cha mabao 7-0 walichoipa Ruvu Shooting kwenye mchezo wa
kwanza msimu huu.
0 comments:
Post a Comment