Saturday, July 21, 2018


Mabingwa wa ligi kuu nchini Uingereza, Manchester City wapo kwenye vita kubwa na klabu ya Everton dhidi ya kuwania saini ya kijana mwenye umri wa miaka 14, Omari Forson.
Forson anayekipiga kwenye klabu ya Tottenham amekuwa kivutio kikbwa cha timu hizo kutokana na uwezo aliyonao katika kufumania nyavu huku saini yake ikihitajika kwa udi na uvumba kwenye dirisha hili la usajili.
Manchester City and Everton are both keeping tabs on Tottenham's Omari Forson – here he is pictured during his time at West Ham
Manchester City na Everton zote zimeshaweka kitita cha fedha mezani kwaajili ya kijana, Omari Forson, picha akiwa na West Ham
Vyombo mbalimbali vya habari vimeanza kumwilika kipaji kikubwa alichojaaliwa Forson ambaye mwenye anandoto za kwenda kufanya mazoezi kwenye klabu ya Everton wiki hii.
Mshambuliaji huyo anayetumia guu la kushoto katika kupachika mabao amekuwa ahihitaji kwenye klabu ya City hata kabla hajaanza kuonekana kipaji alicho nacho alipokuwa na miaka tisa mwaka  2014 alipokuwa West Ham.
Tottenham ilikwenda nyumbani kwa Forson ili kufuatilia maendeleo ya kijana huyo katika kuhakikisha hakuna anayeweza kumsajili.
Forson ambaye wazazi wake ni raia wa Ghana wanao hishi Uingereza amekuwa na mvuto mkubwa kwenye mtandao wa YouTube kutokana na watu wengi kufuatilia video zake zinazo muonyesha akitupia magoli.

0 comments:

Post a Comment