Thursday, August 30, 2018


Usiku wa leo kunatarajiwa kutangazwa droo ya michuano mikubwa kabisa barani Ulaya ya UEFA Champions League ambapo jumla ya timu 32 zikipangwa kwenye makundi.

Maswali mengi yamekuwa yakiibuka juu ya klabu kubwa England, Manchester City, Manchester United, Tottenham Hotspur na Liverpool je zitakutana kwenye hatua hiyo ya makundi.
Wachambuzi wa maswala ya michezo duniani nao wamekuwa wakiangazia je ni grupu lipi litakuwa la kifo kwenye droo hiyo huku mashabiki wa England wakizipa nafasi kubwa klabu ya Liverpool na Manchester City kwenye michuano hiyo.

0 comments:

Post a Comment