Ajenti wa kiungo wa
kati wa Manchester United na Ufaransa Paul Pogba anatarajiwa kuwaambia
Red Devils kuwa anaweza kufikia makubaliano ya pauni milioni 100 kwa
mshindi huyo wa kombe la dunia mwenye umri wa miaka 25 kwenda
Barcelona. (Daily Star Sunday)
Pia
meneja wa Manchester United Jose Mourinho anapanga kuweka siku ya
mwisho kumwinda mlinzi wa England Harry Maguire, 25, ambaye amewekewa
thamani ya pauni milioni 80 na Leicester. (Sunday Express)
Lakini mbio za Manchester United za pauni milioni 35 kwa mlinzi wa Barcelona raia wa Colombia Yerry Mina zimefikia kikomo kwa sababu ya mvutano kuhusu malipo ya ajenti. (Sun on Sunday)
Chelsea watafanya mazungumzona mshambuliaji wa Ubelgiji Eden Hazard siku ya Jumamosi na kumpa mchezaji huyo wa miak 27 mkataba kwa pauni 300,000 kwa wiki kumzuia asijiunge na Real Madrid. (Sunday Times - subscription required)
s
Borussia Dortmund wanakataa kumuuza wing'a mmarekani anayewekewa thamani ya pauni milioni 60 Christian Pulisic, 19, anayetafutwa pia na Chlsea na Bayern Munich. (Mail on Sunday)
Wolves wametoa ofa ya pauni milioni 16 kwa mlinzi wa Besiktas na Croatia Domagoj Vida, 29. (Sabah - in Turkish)
Benfica wameanzisha mazungumzo kumsaini beki wa Manchester United na Italia Matteo Darmian ambaye amewekewa thamani ya pauni milioni 15m. (Sun on Sunday)
Leicester wanakaribia kumsaini wing'a wa Algeria Rachid Ghezzal, 26, kutoka Monaco. Mchezaji hyo amekuwa akiwindwa na Watford na Southampton. (ESPN)
Kiungo wa kati wa Tottenham na Ublegiji Mousa Dembele, 31, amekaa kuelekea Inter Milan. (Sun on Sunday)
Fulham wameuliza kuhusu kumsaini beki Real Madrid mfaransa Theo Hernandez, 20, kwa mkopo. (Mail on Sunday)

0 comments:
Post a Comment