Habari Njema Kwa Watanzania, Sadio Mane Kukosa Mechi ya Ufunguzi Dhidi ya Taifa Stars
Mkufunzi wa Senegal Aliou Cisse amethibitisha kuwa nyota wake wa Liverpool Sadio mane amepigwa marufuku ya mechi moja hivyobasi hatoshiriki katika mechi ya ufunguzi dhidi ya Taifa Stars ya Tanzania nchini Misri.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 27 atakosa mechi ya kundi C dhidi ya Tanzania tarehe 23 mwezi Juni mjini Cairo baada ya kupewa kadi mbili za njano katika mechi ya kufuzu ya Senegal.
''Kutokuwepo kwake hakutatuathiri kwa njia yoyote'' , kocha Cisse aliambia vyombo vya habari vya Senegal kabla ya kuondoka katika kambi yao ya mazoezi katika eneo la Alicante Uhispania kuelekea Misri.
''Ni kweli kwamba uwepo wake ni muhimu sana kwetu lakini bila yeye tuko dhabiti.Shirikisho la soka CAF limeamua hivyobasi hatuna budi'', Cisse aliongezea.
Mane alipewa kadi ya njano katika mechi ambayo Senegal ilipata ushindi wa 1-0 dhidi ya Equitorial Guinea mnamo tarehe 17 Mwezi Novemba 2018 na pia alipokea kadi nyengine ya njano katika mechi ya ushindi wa 2-0 dhidi Madagascar mnamo tarehe 23 mwezi Machi 2019 ijapokuwa haijathibitishwa katika takwimu za mechi za Caf.
0 comments:
Post a Comment