Monday, July 17, 2017



Tafsiri ya ndoa huwa kubwa kulingana na mtu anavyoweza kuitizama katika muono binafsi. Lakini kwa wengi humaanisha kuwa waliopendana wameamua kuweka bayana kuwa wapo tayari kujenga familia halali inayokubalika kwenye jamii na kwenye sheria za nchi na katika imai zao.
Kwa watu maarufu au celebrities hili huwa jambo kubwa zaidi kutokana na namna ambayo tukio kama la ndoa uhesabika kuwa la kipekee na lenye mvuto kutokana na tafsiri ya watu hawa kuwa hawapo tayari kuwa katika mahusiano ya wazi mara nyingi.
Hii hufanya ndoa zao kupokelewa kwa shangwe na kufuatiliwa kwa sababu pia uchochoea mabadiliko kwenye jamii wanazotoka. Wiki hii mchezaji Kevin Yondani alifanikiwa kufunga ndoa na mchumba wake wa muda mrefu Nancy. Katika tafrija hiyo kulikuwa na matukio mengi lakini yafuatayo ni Matukio baadhi  katika Harusi ya Beki kisiki wa Yanga  Kelvin Yondani iliyofanyika Lamada Hotel Jijini Dar es Salaam.

0 comments:

Post a Comment