Imeandikwa na mshabiki wa soka Tanzania.
Shikamoo Haji, naamini unaendelea vizuri na hongera kwa usajili
muliofanya msimu huu hakika ni usajili mzuri na munaonekana wazi mwaka
huu munataka kombe, japo kila mwaka mumedai munataka kombe lakini mwisho
wa ligi munaambulia maneno.
Safari hii upana wa kikosi chenu ni wazi kwamba Simba munataka
ubingwa, na naamini mukiendelea na umoja muliokuwa nao kati ya mashabiki
na klabu kwa hakika mutachukua kombe la ligi msimu huu na makombe
mengine.
Haji wewe ni mtu mzima na naamini wewe una busara na ndio maana Simba
walikuamini na wakakupa usemaji wa klabu, umri wako, busara zako na
weledi wako ni kati ya vitu ambavyo Simba walikuamini na kukupa usemaji.
Lakini sasa Manara wewe ni msemaji wa Simba au mpondaji wa Yanga,
kipindi hiki si mko katika mchakato wa kubadilisha mfumo wa uendeshaji
klabu? Naamini ni kipindi ambacho unatakiwa kufanya sana kazi yako na
kuwapa mashabiki wa Simba elimu kuhusu hili.
Lakini naona uko bize sana kuwasema Yanga, ila pia sio mbaya kwani
Yanga si ni watani wako?huo ndio utani, lakini je kuanza kuwapa
wachezaji wa Yanga majina mara sijui Shilole, uko busy na kuandika vitu
ambavyo haviisaidii Simba na sidhani kama ulilipwa kwa ajili ya hilo.
Mbaya zaidi leo nimeona umepost picha kuhusu mwenyekiti wa Yanga
ambaye kwa sasa yuko matatizoni, Manji ana watoto na ana familia, sawa
yuko matatizoni lakini sisi kama familia ya soka inabidi tuachane na
masuala ya kesi yake na tuzungumzie yetu ya soka, Manji yuko matatizoni
Haji muache.
Haji umeshawahi kujiuliza kama wewe uko matatizoni na mtu mwenzio wa
soka akapost jambo baya kuhusu wewe na akaliunga mkono?hata kama ni
kweli wewe ungejisikiaje? Ungejisikia vizuri?masuala ya walioko
matatizoni na serikali tuwaachie wao sisi tuzungumzie soka.
Wachezaji unaowasema kwa mabaya wengi wana familia, kibaya zaidi
unawasema watu hata hawakujibu, mimi naona hawana muda na wewe au labda
wanakudharau (sijui), mimi naona kama wao hawaoni ngoja mimi tu
nikuambie kwamba fanya kazi yako hayo mengine waachie mashabiki.
Mwisho nakutakia kila la kheri katika kazi yako, nakutakia kila la
kheri katika mchakato munaofunya na mpambane uwanjani mubebe ubingwa
naamini safari hii hamtalia na ubingwa wa mezani kama ulivyotudanganya
mwaka jana kuwa Fifa watawapa.
Home
»
»Unlabelled
» Barua ya wazi kwa Haji Manara
Wednesday, September 13, 2017
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments:
Post a Comment