Thursday, September 28, 2017

Chelsea wameendeleza rekodi yao nzuri dhidi ya timu za Hispania ugenini baada ya leo kuipiga Athletico Madrid mabao 2 kwa 1, Athletico walitangulia kupitia kwa Griezman kabla ya Morata na Batshuayi kufunga mawili.
Mechi kati ya Athletico Madrid Vs Chelsea ilikuwa mechi ya kwanza kwa Athletico kucheza katika uwanja wao mpya wa Wandra Metropolitano katika champions league, mchezo mwingine wa group C ilikuwa kati ya Quarabag vs As Roma huku Manolas na Dzeko wakiifungia Roma.
CSKA Moscow wakiwa nyumbani walikubali kupigwa bao 4 kwa 1 na Manchester United huku Romelu Lukaku akifunga mara mbili,Martial na Mkhtaryan walifunga bao moja moja huku la Moscow likifungwa na Kuachev na kuwafanya United kuongoza kundi A.
Dani Alves, Neyamar na Edison Cavanni waliuua Bayern Munich bao 3 kwa 0, huku Celtic wakiwa ugenini wakiifunga Anderchelt 3 huku mabao ya Celtic yakiwekwa kimiani na Patrick Roberts, Scott Sinclair na Griffiths.
Gonzalo Higuain na Mario Mandzukic waliisaidia Juventus kupata alama 3 katika Champions League huku Barcelona wakizidi kujichimbia ugenini baada ya goli la kujifunga la Sebastian Coates.

0 comments:

Post a Comment