Monday, November 6, 2017

Taarifa rasmi kutoka Simba imethibitisha kiungo wao mshambuliaji Said Hamisi ‘Ndemla’ anaondoka kesho kwenda nchini Sweden kufanya majaribio ya kucheza soka la kulipwa.
Atafanya majaribio hayo kwenye klabu ya AFC Eskilstuna inayoshiriki ligi kuu nchini Sweden. Majaribio hayo ni ya wiki mbili (siku 14).
Eskilstuna ndio klabu ambayo anakipiga mtanzania mwingine Thomas Ulimwengu ambaye kwa sasa anauguza jeraha la goti baada ya kufaniwa upasuaji.

0 comments:

Post a Comment