Na Priva ABIUD.
Ni miaka 6 imepita tokea mkurugenzi wa zaman wa Ac Milan bwana Adriano Galliani afanye kosa aliloliita kosa lake la maisha. Ni pale alipomruhusu kiungo bora kabisa Andrea Pirlo kujiunga na mahasimu wao wakubwa Juventus. Kosa alilolifanya Gallian kwa sasa linamtesa mkurugenzi mkuu wa Millan kwa sasa Marco Fassone ambaye ameingia mgogoro mkubwa na Wakala wa Golikipa wa klabu hiyo Gianluigi Donnarumma kwa kila kinachoitwa vita ya pesa. Donnaruma anahitaji kuondoka.
Donnarumma
mlinda mlango kwa Ac Milan kwa sasa anaishi kama mkimbizi ndani ya
taifa lake. Hivi majuzi tu kwenye mchezo wa timu taifa ya vijana ya
Italia Donnarumma alitupiwa hela feki na mashabiki kwa kile walichodai
kuwa bwana mdogo aligomea mshahara wa E80,000 kwa wiki akiwa na miaka 18
tu. Mino Raiola aliyekuwa dalali wa dili la Paul Pogba, ndiye wakala wa
Donnarumma, na alikanusha kuwa mteja wake kuwa hakusaini kwa sababu za
kifedha. Raiola ilisema alihofia usalama wa mteja wake klabuni hapo.
Donnaruma alijiunga Ac milan akiwa na miaka 16 akiwa anapata mshahara wa
E100,000 kwa mwaka.Amejipatia umaarufu mkubwa kwa uwezo wake akiwa golini. Baada ya sekeseke kuisha Donna alisaini mkataba mpya ambapo alikuwa akipokea Euro milion 6 kwa mwaka. Lakini bado inaonekana ugonjwa ule umerudi tena. Mino Raiola anamwekea kijana huyu mazingira magumu sana. Mino amesikika mara kadhaa akilalamika kuwa Donnarumma haheshimiki na baadhi ya Vipengele vya mkataba wake havilindwi.
Donnaruma
alisaini mkataba mpya mpaka 2012. Pia Ac Milan ilimsajili kaka yake.
Kivumbi kilianza kwenye mchezo wa Copa Italia dhidi ya Verona ambapo
mashabiki uwanja mzima walikuwa wakimzomea. Donnarumma alijikuta akitoa
machozi San Siro. Mashabiki wa Ac Milan ni wakorofi sana. Hawana
uvumilivu. Wamekosa uvumilivu wa kisoka. Bado chuki za kuporomoka kwa
soka lao linawapa stresi. Inafika steji wanaanza kuwatukana hadi
wachezaji wao wazawa wanapotaka kulinda maslahi yao.Mashabiki wamekaa kwenye viti na mabango kumzomea mtu aliyejitolea maisha yake kulinda furaha yao lakini bado wanamtukana. Walio wengi wanamtukana Donnaruma wanasema kuwa anapenda hela kuliko klabu ya Ac Milan.
Kwa
akili ya kawaida ni nani hapendi pesa? Yuda Iskarioti mwenywe alimuuza
Mwana wa Mungu kisa pesa. Makanisa mengi duniani yanahimiza matoleo ya
sadaka, wewe ni nani kama viongoz wa dini wanatuhubiria kuhusu sadaka?
Hivi unajua kazi anayoifanya Donnaruma pale golini? Yaani mtu anajitupa
kufuata mashuti ya watu mnasema anapenda hela? Mlitaka apende nini? Cha
muhimu katika maisha ya mchezaji kwanza ni maslahi yake. Huwezi
kutegemea kazi ya mchezaji bila kutimiza maslahi yake.Nawashangaa sana Mashabiki wa Ac Milan ambao wamepoteza muda wao wakizunguka mitaa ya Santa Maria Dele gracie kwenye steshenari za Fabriano Boutique, Pettinaroli na wengine wakijazana maduka ya San Maurilio na Pasini Milano kutengeneza hela bandia ili wakamtupie Donnoruma.
Kwan
wanadhani Donnarumma hapendi maisha mazuri? Hivi ni kweli kwamba
hapendi kutembelea Buggati Veryon na kupumzika hoteli za kifahari kama
Pallazo Parigi kule milano? tena kwenye vyumba vya gharama kabisa? Nae
anapenda kwenda fukwe za Puglia na San Vitolo Capo kule sicily kula
bata wakati wa mapumziko na familia yake. Yaani kwa akili yao wanafikiri
Donnarumma anapopigiwa mashuti golini na kudaka kama mtu asiye na akili
kwamba hawazi maisha mazuri? KAMA DONNARUMA ATAKUBALI KUONDOKA NDANI
YA TAIFA LAKE ATAJIJENGEA UADUI MKUBWA SANA KWA WAITALIANO NA ATAPOTEZA
HESHIMA YAKE. ACHAGUE POCHI LA RAIOLA AU MAKOFI YA HESHIMA SAN SIRRO.
Narudia tena heshima zipo jeshini kwenye soka cha kwanza maslahi. Siku
njema

0 comments:
Post a Comment