
Ujumbe wa twitter
uliotumwa na Bernardo Silva kwa mchezaji mwenza wa timu ya Manchester
City, Benjamin Mendy unachunguzwa na shirikisho la soka kwa kutuhumiwa
kuwa wa ubaguzi.
Mchezaji wa timu ya taifa ya Ureno Silva
alimlinganisha Mendy na kibonzo cha rangi ya chakuleti kwenye pakiti ya
pipi ya Conguitos - zinazopatikana Uhispani na Ureno.Ujumbe huo uliwekwa Jumapili mwendo wa saa tisa kasoro robo mchana na ukafutwa mwendo wa saa tisa na nusu.
Baadaya hapo Bernardo alituma ujumbe mwingine kwenye twitter: "Huwezi hata kufanya mzaha siku hizi na rafiki yako."
Mashabiki walijibu kwa kutaka ujumbe huo ufutwe.
Mmoja aliandika "Mshkaji, amekutusi kwa ubaguzi wa rangi." Mwingine aliandika: "Bernado Silva ameandika ujumbe gani?"
- Manchester City yairarua Watford bila huruma
- West Ham yaishinda nguvu Man United
- Je Mourinho kuchukua mahala pake Zidane?
Mendy alijibu ujumbe huo na hakuonekana kuhisi vibaya.
Manchester City imekataa kutoa tamko kuhusu hilo.
FA litaukagua ujumbe huo na msingi wa kwanini uliandikwa hadharani kabl aya kuamua hatua ya kuchukua.
0 comments:
Post a Comment