Friday, January 10, 2020

Gareth Bale
Real Madrid bado inataka kumuuza mshambuliaji wa kimataifa wa Wales Gareth Bale, 30, licha ya ajenti wake kutilia shaka uhamisho wake msimu wa joto. (Telegraph)
Chelsea imeungana na Tottenham kumsaka winga wa Ufaransa Thomas Lemar, 24, kwa mkopo kutoka Atletico Madrid hadi mwisho wa msimu huu. (Telegraph)
Manchester United wamekubali kuwa haitafanikiwa kumleta Old Trafford kiungo wa kati wa Tottenham Christian Eriksen, 27. (Evening Standard)
Christian Eriksen
Spurs wanatafakari uwezekano wa kumsaini mshambuliaji wa zamani wa Celtic Moussa Dembele, 23, kutoka Lyon baada ya kubaini kuwa Harry Kane hatakuwa uwanjani hadi Aprili baada ya kujeruhiwa. (Goal)
Tottenham wamefikia mkataba wa £28m kumnunua mshambuliaji wa AC Milan na Poland Krzysztof Piatek, 24. (Sun)
Spurs wanamtaka beki wa Barcelona na Portugal Nelson Semedo, 26. (Mirror)
Krzysztof Piatek
Mkufunzi wa West Ham, David Moyes anataka kumsaini kiungo wa kati wa Ubelgiji Marouane Fellaini, 32, kutoka Shandong Luneng. (Sky Sports)
Leicester haijakatiza matumaini ya kumsajili beki wa Juventus na Uturuki Merih Demiral, 21, licha ya ofa zao mbili kukataliwa na pamoja na ushindani kutoka Manchester City. (Mirror)
Mkufunzi wa zamani wa Arsenal Unai Emery amefichua kuwa Everton ilimhoji kwa saa tatu kuhusu usimamizi wa klabu hiyo kabla ya kumuajiri Carlo Ancelotti. (Mail)
Arsenal Unai Emery
Arsenal wako mbioni kumsaka beki Yan Couto, 17, kutoka klabu ya Brazil ya Coritiba. (Globoesporte - via Metro)
Barcelona itamenyana na Arsenal kumsajili beki wa RB Leipzig na Ufaransa wa chini ya miaka -21 Dayot Upamecano, 21. (Express)

Tetesi Bora Alhamisi

Arsenal na Manchester United wamewasilisha ofa ya kumsajili mshambuliaji wa Paris St-Germain na Uruguay Edinson Cavani, 32. (El Chiringuito - via Metro)
Arsenal Unai Emery
Chelsea sasa wanamlenga mlinzi wa West Ham Issa Diop na wanatazamiwa kutuma dau la usajili la pauni milioni 40 kwa Mfaransa huyo mwenye miaka 22. (Express)
Manchester United wanaaminika kutaka kumsajili beki wa klabu ya Hellas Verona ya Italia na raia wa Albania Marash Kumbulla, 19. (Star)
Ajax wanapanga kumrudisha beki Matthijs de Ligt, 20, kwa mkopo licha ya kumuuza mchezaji huyo licha ya kumuuza Juventus mwishoni mwa msimu uliopita. (A Bola - in Portuguese)
Matthijs de Ligt
Chelsea inaonekana haipo tayari kumsajili mshambuliaji wa Crystal Palace na timu ya taifa ya Ivory Coast Wilfried Zaha, 27, huku meneja Frank Lampard akiona mchezaji huyo haendani na kikosi chake. (90min)
Crystal Palace wamekataa kumuuza Zaha kwa vigogo wa Ujerumani Bayern Munich. (Guardian)

0 comments:

Post a Comment