BEKI Muitalia, Marco Materazzi, amemchana
vibaya kocha wake wa zamani, Rafael Benitez.
Wawili hao walikutana
kwenye kikosi cha Inter, ikiwa ni baada ya mwaka 2010 timu hiyo kuchukua
ubingwa wa Ligi ya Mabingwa Ulaya chini ya Kocha Jose Mourinho.
"Ndani ya Inter, siyo
kwamba Benitez utawala wake ulianza vibaya na kumalizika vibaya, bali haukuisha
kabisa.
"Alitibua kila kitu
ambacho Mou [Jose Mourinho] alikijenga.
"Alipofika
alijaribu kuwaweka kando wale wote ambao walionekana kuwa na sauti katika
chumba cha kubadilishia nguo, hapo ndipo shida ilipoanzia," alisema Materazzi.
![]() |
Materazzi akishangilia na Mourinho. |
Beki huyo wa zamani wa Everton, alimsifia Mourinho kwa kumtolea mifano Benitez kwamba alishinda kutatua matatizo.
"Kipindi cha Mourinho
wote tulikuwa na ushirikiano.
"Alifanya mambo
makubwa yenye faida. Kama mtu anapenda kuondoa yale ya zamani na kuleta mambo
mapya kwa ajili ya faida ya klabu, namuheshimu, lakini Benitez alijaribu tu
kuondoa kila kitu cha Jose, hiyo ilitusumbua.
"Mtu ambaye
ameshinda ubingwa wa Ligi ya Mabingwa Ulaya akiwa na Liverpool mbele ya Milan
lazima atakuwa na uelewa wa hali ya juu, lakini ndani ya Inter, Benitez alikuwa
na matatizo makubwa na mimi, alipoenda Napoli akasumbuana na Paolo Cannavaro,
kule Chelsea ugomvi ukawa na John Terry, Real Madrid alikorofishana na Cristiano
Ronaldo.
0 comments:
Post a Comment