Thursday, June 22, 2017




Details
Created: Thursday, 22 June 2017 05:21


 

 >LEO CAMEROON-AUSTRALIA & GERMANY-CHILE!
JANA Mexico walitoka nyuma na kuifyeka New Zealana Bao 2-1 kati Mechi yao ya Pili ya Kundi A la Mashindano ya FIFA ya Kombe la Mabara ndani ya Fisht Stadium Jijini Sochi huko Nchini Russia.
Mapema Jana, katika Mechi nyingine ya Kundi A, Portugal iliwafunga Wenyeji Russia 1-0 kwa Bao la Cristiano Ronaldo.
Hizo zilikuwa ni Mechi za Pili kwa kila Timu katika Kundi A na kuzifanya Mexico na Portugal zifungane uongozini zikiwa na Pointi 4 kila moja lakini Mexico wako juu kwa Mabao, Watatu ni Russia wenye Pointi 3 na mkiani ni New Zealand ambao tayari washaaga Mashindano.
Timu 2 za juu za kila Kundi zitasonga Nusu Fainali.
New Zealand walitangulia kufunga katika Dakika ya 42 kwa Bao la Chris Wood, anaecheza England na Klabu ya Leeds United, lakini Mexico, ambao Jana Kocha wao Juan Carlos Osoria alibadili Wachezaji 8 toka kile Kikosi kilichotoka Sare 2-2 na Portugal akiwemo Javier Hernandez ‘Chicharito’, walijibu Kipindi cha Pili na kufunga Bao 2.
Bao za Mexico zilifungwa na Raul Jimenez na Oribe Peralta.
++++++++++++++++

++++++++++++++++
Mechi hii ilikumbwa na mzozo mwishoni wakati Diego Reyes Nahodha wa Mexico alipomvuta Michael Boxall na kisha Hector Herrera kuingilia nah apo Ryan Thomas wa New Zealand kuvamia sakata hilo.
Refa Bakary Gassama kutoka Gambia akaitisha msaada wa VAR, Video Assistant Referee. Na baadae kutoka Kadi za Njano 3 kwa Reyes, Herrera na Boxall.
Leo zipo Mechi 2 za Kundi B ambazo zitakuwa Mechi za Pili kwa kila Timu, wakati Cameroon wataanza na Australia na kisha Mabingwa wa Dunia Germany kucheza na Chile.
VIKOSI VILIVYOANZA:
NEW ZEALAND (Mfumo 5-3-2): Marinovic; Ingham, Boxall, Durante, Smith, Wynne; McGlinchey, Rojas, Thomas; Lewis, Wood.
Akiba: Brotherton, Tzimopoulos, Tuiloma, Barbarouses, Smeltz, Moss, Patterson, Doyle, Colvey, Rufer, Roux, Williams.
MEXICO (Mfumo 3-5-2): Talavera; Salcedo, Araujo, Alanis; Damm, D. Reyes, G. Dos Santos, Fabian, Aquino; Jimenez, Peralta
Akiba: Cota, Marquez, J. Dos Santos, Layun, Vela, Ochoa, Hernandez, Moreno, Herrera, Guardado, R. Reyes, Lozano
REFA: Bakary Gassama [Gambia]
++++++++++++++++
FIFA KOMBE LA MABARA
Ratiba/Matokeo:
Hatua ya Kwanza
Jumamosi Juni 17
KUNDI A
Russia 2 New Zealand 0
Jumapili Juni 18
KUNDI A
Kazan Arena, Kazan
Portugal 2 Mexico 2
KUNDI B
Spartak Stadium, Moscow
Cameroon 0 Chile 2
Jumatatu Juni 19
KUNDI B
Australia 2 Germany 3
Jumatano Juni 21
KUNDI A
Russia 0 Portugal 1
Mexico 2 New Zealand 1
Alhamisi Juni 22
KUNDI B
Saint Petersburg Stadium, Saint Petersburg
1800 Cameroon v Australia
Kazan Arena, Kazan
2100 Germany v Chile
Jumamosi Juni 24
KUNDI A
Kazan Arena, Kazan
1800 Mexico v Russia
Saint Petersburg Stadium, Saint Petersburg
1800 New Zealand v Portugal
Jumapili Juni 25
KUNDI B
Fisht Stadium, Sochi
1800 Germany v Cameroon
Spartak Stadium, Moscow
1800 Chile v Australia
Hatua ya Pili
Nusu Fainali
Jumatano Juni 28
Kazan Arena, Kazan
2100 Mshindi Kundi A v Mshindi wa Pili Kundi B [NF1]
Alhamisi Juni 29
Fisht Stadium, Sochi
2100 Mshindi Kundi B v Mshindi wa Pili Kundi A [NF2]
Mshindi wa 3
Jumapili Julai 2
Spartak Stadium, Moscow
1500 Atakaefungwa NF1 v Atakaefungwa NF2
FAINALI
Jumapili Julai 2
Saint Petersburg Stadium, Saint Petersburg
2100 Mshindi NF1 v Mshindi NF2

0 comments:

Post a Comment