na alanus
Klabu hiyo imethibitisha kwenye mitandao ya kijamii kwamba atafanyiwa uchunguzi wa kimatibabu kabla yake kutia saini mkataba Ijumaa.
Clichy alijiunga na City kutoka Arsenal mwaka 2011, na alishinda mataji ya Ligi ya Premia mara mbili na kombe moja la EFL akiwa na klabu hiyo.
Maelezo zaidi kuhusu kuhamia kwake Uturuki hayajatolewa lakini taarifa Uturuki zinasema huenda beki huyo atalipwa euro 3m (£2.6m) kila msimu na kwamba mkataba wake ni wa miaka mitatu.
Clichy atajiunga sana na mshambuliaji wa zamani wa City na Arsenal Emmanuel Adebayor ambaye alijiunga na Istanbul Basaksehir mwezi Januari.
Klabu hiyo ilimaliza ya pili ligi kuu ya Uturuki msimu uliopita, ambapo Adebayor aliwafungia mabao sita ligini.
0 comments:
Post a Comment