Inasemekana timu ya taifa ya Argentine imefutilia mbali mchezo wao wa kirafiki dhidi ya taifa la Israel. Taifa hilo lilipata ripoti kwamba Lionel Messi na mke wake walipokea vitisho kutoka kwa wapalestine wakiwataka kuahirisha mchezo huo mara moja.
Katibu mkuu wa chama cha soka cha Palestina Jibril Rajoub aliuomba uongozi wa chama soka cha argentine kufuta mchezo huo mara moja
Baadhi ya mashabiki wa Messi nchini Palestina walichoma jezi za nyota huyo mara baada ya kikosi hicho kuwasili Jerusalem kwa muda.
Rajoub amesema anafahamu wazi kuwa mchezo huo ulikuwa ni wa kusheherekea Miaka 70 ya shirikissho la soka nchini humo.
Waziri mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu aliwasiliana na Rasi wa Argentine Mh Mauricio Macri. Netanyahu alimsihi Sana Macri kuwahimiza uongozi na wachezaji kutokufutilia mbali mchezo huo siku ya jumanne. Macri alimjibu waziri huyo kuwa yeye hawezi kuingilia maamuzi ya mwisho ya chama cha soka cha taifa hilo.
Raisi Macri aliwasiliana na uongozi wa chama cha soka kujua msimamo wao. Viongozi walimwambia kuwa kila mchezaji ana hofu na hakuna mchezaji ambaye yupo tayati kucheza pambano hilo. Macri alimpigia simu waziri wa Israel na kumuomba radhi kwamba hakuna mchezaji ambaye atakubali kucheza pambano hilo.
Macri mwenyewe alikuwa tayari kwenda katika mpambano baada ya kualikwa na matajiri wa kiyahudi wanaofanya kazi.
Mchezaji wao Gonzalo ” Nashukuru kwa maamuzi hayo Kwa ajili afya zetu na maisha yetu. Hakukua na haja ya kucheza na wayahudi.
Hata hivyo Uongozi wa chama cha soka cha Israel kimishtumu sana maamuzi ya Rajoub na kusema amevunja mipaka.
Waziri wa Ulinzi wa israel Avigdor Lieberman amelaani kitendo hicho na kudai kuwa Wapalestina wamejaa chuki na wivu.
Msemaji wa wizara ya ulinzi Gilad Erdan alionhelea suala hilo na kusema kwamba
wamekuza jambo hilo kwa makusudi ili kumtisha Messi. Amesema kitendo cha kuchoma jezi za nyota huyo ni mipango ya taifa hilo kutaka kuondoa amani.
0 comments:
Post a Comment