Leo Jumanne kutakuwa na mechi nyingine ya kundi C kati ya
Australia na Peru itakayochezwa katika uwanja wa Flsht Olympic uliopo
mji wa Sochi.
Australia: walikuwa na mwanzo mzuri wa mashindano na ilipelekea
kukosa pointi dhidi ya Ufaransa baada ya kujifunga goli katika dakika za
mwisho na kuambulia pointi moja dhidi ya Denmark, katika mechi
iliyoisha 1-1. Kwa hali yoyote wanajua kwamba ushindi tu wa magoli mengi
ndo utafanya wawe na nafasi ya kuwashinda Denmark kwenye msimamo wa
kundi C na kuingia hatua ya 16 bora kwa mara ya kwanza katika miaka 12.
Hivyo Australia wanaomba Ufaransa wamfunge Denmark.
Tim Cahil alikuwa sehemu ya kikosi kilichofanikiwa Ujeruman mwaka
2016, na anaweza kucheza kwa mara ya kwanza katika kombe lake la dunia
ambalo litakuwa la mwisho kwake.Anategemea kuanza kutokana na Andrew
Nabbouts kuteguka bega ambapo alilipata dhidi ya Denmark. Jamie Maclaren
au kijana anayevutia Tomi Juric anaweza kuchukua nafasi ya Nabbout
katika safu ya mbele.
Peru: Waamerika ya kusini wameshatolewa tayari baada ya kupoteza
mechi yao dhidi ya Ufaransa na Denmark. Kwa hali yoyote watakuws na
matumaini ya kumaliza safari yao ya Urussi huku wakitegemea kupata
ushindi ili kuweka sifa kwenye timu.
Upande wao utakuwa bila mshambuliaji wao Jefferson Falfan baada ya
nchezaji huyo wa Lokomotiv Moscow kuumia kichwa kwenye mazoez. Alikuwa
benchi dhidi ya Ufaransa.Hivyo Paulo Guerrero anatakiwa kuendelea kuwa
mtu pekee wa Peru katika safu ya ushambuliaji.
Mitazamo ya makocha wa timu zote mbili
Australia: Kocha wa Australia Bert Van Marwijk akizungumza kuelekea kwenye maandalizi ya mchezo;
Najua kwamba Peru ni timu nzuri na wameonyesha hapa Russia. ” Wanacheza
kwa hisia, wana hatari zaidi na tunatakiwa kuwa kitu kimoja.
” Mechi ni muhimu kwetu. Tunaichukukulia umuhimu hasa hasa kwa
waliotufata hapa na wanaorudi nyumbani, ambao wamekuwa pamoja nasi kwa
moyo wote.
Kocha wa Peru Ricardo Gareca amesema
” Mechi ni muhimu kwetu.”
” Tunaichukulia kama ni ya muhimu kwetu.Tunataka kumaliza ushiriki wetu hapa kwa namna yake hasa kwaajili ya mashabiki wetu.
Kumbukumbu
Hii ni mara ya kwanza timu hizi mbili zinakutana, lakini Peru
waliwafunga majirani wa Australia, Newzealand katika mechi za kufuzu za
kombe la dunia.
Nahodha wa Peru Paolo Guerrero alikuwa anakosa kombe la dunia baada
ya kupewa adhabu ya matumizi mabaya ya dawa baada ya kunywa chai
iliyochanganywa na Coca leaf lakini adhabu ilipunguzwa kutoka miezi 18
mpaka miezi 6.
Vikosi vinavyoweza kuanza
Australia: Ryan, Risdon, Sainsbury, Milligan, Behich, Jedinak, Mooy, Leckie, Rogic, Kruse, Juric
Peru: Gallese, Trauco, Rodriguez, Ramos, Advincula, Yotun, Tapia, Froles, Cueva, Carillo, Guerrero.
Home
»
»Unlabelled
» RUS 2018: Tanga Mpo? Wapinzani wa Poulsen
Tuesday, June 26, 2018
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments:
Post a Comment