Wednesday, July 25, 2018

Hugo Lloris
Real Madrid inajiandaa kutoa dau la £60m kumnunua mlinda lango wa Tottenham na Ufaransa Hugo Lloris, 31. (Sun)
Bilionea wa Urusi Alisher Usmanov anataka kuuza asilimia 30 ya hisa zake katika klabu ya Arsenal baada ya kukiri kwamba mmiliki mkuu wa klabu hiyo Stan Kroenke hatomwachia udhibiti wa klabu hiyo. (Financial Times)Thaigo Alcantara
Manchester United na Chelsea zimewasilisha ombi la kutaka kumsaini kiungo wa kati wa Bayern Munich na Uhispania Thiago Alcantara, 27, ambaye anapatikana kwa dau la £62m. (ESPN)
Haki miliki ya picha Getty Images
United pia inajiandaa kuwasaini mchezaji mbadala wa winga wa Chelsea na Brazil Willian,kupitia winga wa croatia na Eintracht FrankfurtAnte Rebic, 24. (Independent)
Tottenham na Chelsea huenda zikamnyatia winga wa Ufaransa Anthony Martial, 22, ambaye anataka kuondoka katika klabu ya Manchester United lakini kusalia katika ligi ya Premia. (Sun)
Chelsea huenda ikamkosa mshambuliaji wa Juventus Gonzalo Higuain, 30, huku wapinzani wao wa Serie A AC Milan wakiwa na hamu ya kumsajili raia huyo wa Argentina kwa dau la £57m. (Evening Standard)
Anthony Martial
Chelsea inakaribia kumsaini mlinda lango wa siku nyingi wa Uingereza Robert Green, 38, kama nguvu mpya kwa uhamnisho wa bure. (Sun)
Fulham imekubali makubaliano ya kumsaini mchezaji wa Ujerumani na winga wa zamani wa Chelsea Andre Schurrle, 27, kutoka Borussia Dortmund. (West London Sport)
Liverpool itamzuia mshambuliaji Daniel Sturridge, 28, msimu huu na iko tayari kumpoteza mchezaji huyo wa Uingereza msimu ujao kwa uhamisho wa bure (Liverpool Echo)
Haki miliki ya picha Getty Images
Everton na West Ham wana hamu ya kumsaini beki wa Augsburg na Austria Martin Hinteregger, 25, ambaye ana thamani ya £13m. (Sun)
Wolves wanatarajiwa kumsaini winga wa Uhispania Jonny Castro, 24, kwa mkopo wa muda mrefu kutoka knblau ya Atletico Madrid. (Mail)
Derby imeanza mazungumzo ya kutaka kumsaini mshambuliaji wa Uingereza mwenye umri wa miaka 28 Martyn Waghorn kutoka klabu mwenza ya ligi ya mabingwa Ipswich kwa dau la £8m. (Mail)
Haki miliki ya picha Getty Images
Werder Bremen imefanya uchunguzi kuhusu kumsaini kiungo wa kati wa Everton na Uholanzi , 25, Davy Klaassen. (SkySports)
Fenerbahce wamewasilisha ombi la kumsaini mshambuliaji wa Tottenham na Uholanzi Vincent Janssen, 24, ambaye alihudumu msimu uliopita kwa mkopo katika klabu hiyo ya Uturuki . (SkySports)
Haki miliki ya picha Getty Images
Celtic inapanga mazungumzo ya dharura ya kuandikisha mkataba na beki Dedryck Boyata, 27, licha ya hamu ya kumsaini raia huyo wa Ubelgiji kutoka kwa klabu za Fulham na Lyon. (Daily Record)
Mkufunzi wa zamani wa Uingereza Sven-Goran Eriksson, 70,ameanza mazungumzo ya kuchukua ukufunzi wa timu ya taifa la Iraq. (Sky Sports)

Tetesi za soka Ulaya Jumanne 24.07.2018

Theirry Henry
Mshambuliaji wa zamani wa Arsenal Thierry Henry, ambaye yuko katika kikosi cha ukufunzi cha Ubelgiji amekubali kwa maneno kuchukua uoingozi wa klaby ya Aston Villa akichukua mahala pake Steve Bruce. (Daily Star)
Chelsea inajiandaa kuimarisha dau la £45m kumnunua beki wa Juventus na Itali Daniele Rugani, 23, baada ya ombi la hapo awali la £36m kukataliwa. (Goal)
Willian
Chelsea imekataa ombi la tatu la zaidi ya £55m - kutoka Barcelona kumnunua winga wa Brazil Willian, 29. (Sky Sports)
Arsenal bado ina hamu ya kumsajili kiungo wakati wa Sevill aliyeshinda kombe la dunia Steven Nzonzi, 29,lakini hawako tayari kuafikia matakwa ya kandarasi ya raia huyo wa Ufaransa ya kumuachilia kwa dau la £35m. (France Football)
 Anthony Martial
Mkufunzi wa Manchester United Jose Mourinho anapanga kumpiga bei winga wa Ufaransa Anthony Martial, 22, kwa dau la £50m lakini kwa klabu ambayo haichezi ligi ya Uingereza. (Guardian)
Tottenham ina matumaini ya kujipatia £30m kupitia kumpiga bei mshambuliaji wa Uholanzi Vincent Janssen, 24, pamoja na mshambuliaji wa Uhispania Fernando Llorente, 33. (Evening Standard)
Newcastle iko katika mazungumzo kumsajili beki wa Deportivo La Coruna na Uswizi Fabian Schar, 26, ambaye ana kandarasi inayomzuia yenye thamani ya £3.5m . (Daily Mail)
Luca Digne
Everton inamtaka beki wa Barcelona Lucas Digne lakini imepunguza hamu yao kwa beki wa kushoto wa Scotland Kieran Tierney. Raia wa Ufaransa Digne, 25, ana thamani ya £22m. (Liverpool Echo).
Klabu mpya iliopanda katika ligi ya Premia Fullham imewasilisha ombi la kutaka kumnunua mshambuliaji wa Brazil na Real Sociedad Willian Jose, 26 kwa dau la £26m. (Sun)
Haki miliki ya picha Getty Images
Kipa wa Uhispania Fabri, 30, amefanyiwa vipimo vya kimatibabu katika klabu ya Fullham akisubiri uhamisho wake wa dau la £5m kutoka klabu ya Uturuki ya Besiktas. (Sky Sports)
West Ham na Leicester zote zinamnyatia kiungo wa kati wa Juventus na Itali ,25, Stefano Sturaro. (La Gazzetta dello Sport - in Italian)
Haki miliki ya picha Getty Images
Real Madrid ina hamu ya kumsajili kiungo wa kati wa Borussia Dortmund na Marekani Christian Pulisic, 19, ambaye ana thamani ya £60m. (Daily Mail)
Barcelona, Juventus na idadi kubwa ya klabu za Premia zinamtaka winga mwenye umri wa miaka 20 Ismaila Sarr. Rennes inataka kulipwa £50m ili kumpiga bei mchezaji huyo wa Senegal (Sun)
West Brom wanakaribia kumnunua kiungo wa kati wa Uingereza Harvey Barnes, 20, kwa mkopo kutoka Leicester. (Leicester Mercury)

0 comments:

Post a Comment