Karibia Ligi Kubwa zote barani Ulaya tayari zimeshaanza msimu mpya wa mwaka 2018/19 na jana usiku tulishudia Ligi Kuu Soka Hispania (La Liga) na Ligi Kuu Soka Italia (Serie A) zikianza kutimua vumbi.
Lionel Messi akitupia goli 2 peke yake huku la tatu likifungwa na Philippe Coutinho, matokeo ambayo yameifanya Barcelona ikae kileleni kwenye msimu wa La Liga.
Kule Italia nako mchezo mkali ulikuwa ni wa Chievo Verona dhidi ya Juventus, mchezo ambao uliisha kwa Juventus kuibuka na ushindi wa goli 3-2 .
Kule Ufaransa nako wakati Messi akifanya yake Hispania, Kylian Mbappe naye aliwanyanyua mashabiki wa PSG baada ya kutupia magoli mawili dhidi ya Guingamp katika mchezo wake wa kwanza tangu atoke kwenye fainali za Kombe la Dunia .
0 comments:
Post a Comment