Friday, September 11, 2020


Pierre-Emerick Aubameyang, 31
Maelezo ya picha,

Mshambuliaji wa Arsenal na Gabon Pierre-Emerick Aubameyang, 31

Mshambuliaji wa Arsenal na Gabon Pierre-Emerick Aubameyang, 31, atasaini mkataba mpya wa miaka mitatu na klabu hiyo utakaomfanya kuwa mchezaji anayelipwa zaidi klabuni hapo. (Athletic - subscription required)

Mshambuliaji wa Tanzania, Mbwana Samatta, 27, ataweza kuondoka Aston Villa miezi minane tu baada ya kujiunga na klabu hiyo. (Mail)

Chelsea imekataa ofa ya Inter Milan kwa ajili ya kiungo wake aliyetwaa kombe la dunia N'Golo Kante, 29, ofa ambayo inajumuisha kubadilishana na kiungo wa Croatia Marcelo Brozovic, 27. (Guardian)

Mlinzi wa Manchester United Muingereza Chris Smalling, 30, hajahudhuria mazoezi wiki hii akikaribia kutua ligi ya Italia, Serie A, kwenye timu ya Roma, kwa uhamisho wa kudumu, timu ambayo aliichezea kwa mkopo msimu uliopita.(Telegraph - subscription required)

Ngolo Kante

Kiungo wa Liverpool Georginio Wijnaldum, 29, amefanya mazungumzo yaliyoenda vizuri na meneja Jurgen Klopp kuhusu mustakabali wake klabuni hapo. Mholanzi huyo amebakiza mwaka mmoja kwenye kandarasi yake ya sasa pale Anfield. (Sky Sports)

Beki wa England na Tottenham Rose, 30, anakaribia kutimka ligi kuu ya Uingereza kujiunga na kikosi cha Serie A Genoa.(PA, via Team Talk)

Kipa wa Arsenal Muargentina Emiliano Martinez, 28, amekubali kandarasi ya miaka mine na Aston Villa, yenye thamani ya £60,000 kwa wiki, wakati huo vilabu hivyo vikitarajiwa kukubaliana ada ya uhamisho ya zaidi ya £15m. (Independent)

Kiungo wa Manchester United na Brazil Fred, 27, amepuuza ripoti kwamba anaweza kuondoka msimu huu na kujiunga Galatasaray na Uturuki. (Four Four Two)

Kiungo wa kati wa Brazil Fred
Maelezo ya picha,

Kiungo wa kati wa Brazil Fred

West Brom wako kwenye mazungumzo ya kumnasa mlinzi wa zamani wa Chelsea Branislav Ivanovic, 36, kwa uhamisho huru baada ya kutemwa na Zenit St Petersburg ya Urusi.(Telegraph - subscription required)

Kiungo wa zamani wa Manchester United Ravel Morrison, 27, yuko kwenye mazungumzo na klabu za Uholanzi za Vitesse Arnhem na Utrecht baada ya kutemwa na Sheffield United. (Mail)

Mshambuliaji wa Liverpool na Wales Ben Woodburn, 20, anatarajiwa kujiunga na Sparta Rotterdam Uholanzi kwa mkopo wa muda mrefu wa msimu mzima. (Standard)

Ofa ya Newcastle ya £32m imekataliwa na Lille kwa ajili ya kumsaini kiungo wa Ufaransa mwenye umri wa miaka 21, Boubakary Soumare. (Fabrizio Romano)

kiungo wa Ufaransa mwenye umri wa miaka 21, Boubakary Soumare.
Maelezo ya picha,

kiungo wa Ufaransa mwenye umri wa miaka 21, Boubakary Soumare.

Fulham inataka kumsajili kiungo wa kireno, kutoka Benfica, Florentino Luis, 21, kwa mkopo wa muda mrefu kwa sharti la kumsajili moja kwa moja kwa ada ya £27m. (Sun)

Porto imekataa ofa ya £22m kutoka Wolves kwa ajili ya kiungo wake Jesus Corona. Mkata wa nyota huyo wa Mexico mwenye miaka 27 una kipengele kinachotaka mpaka ilipwe ada ya £27m ndiyo aweze kuhama. (Mail)

TETESI ZA SOKA ALHAMISI

Mshambuliaji wa Tanzania na Aston Villa Mbwana Samatta
Maelezo ya picha,

Mshambuliaji wa Tanzania na Aston Villa Mbwana Samatta

Mshambuliaji wa Aston Villa na Tanzania Mbwana Samatta huenda akaondoka katika klabu hiyo licha ya kujiunga nayo mwezi Januari. Mkufunzi wa klabu hiyo Dean Smith anataka kukifanyia mabadiliko kikosi chake kabla ya dirisha la uhamisho kufungwa.{ Mail Online }

Barcelona imewasiliana na Arsenal kuhusu uhamisho wa beki wa kulia Mhispania Hector Bellerin, 25. (Sport - in Spanish)

Mabingwa wa Ufaransa Paris St-Germain pia wanamtaka Bellerin na imeshawasiliana na wawakilishi wake. (Independent)

Real Madrid wako tayari kulipa nusu ya mshahara wa mwaka wa Gareth Bale ili kusaidia mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 31 raia wa Wales kuondoka katika timu hiyo ya Hispania. (Telegraph - subscription required)

Mshambuliaji wa Everton na Italia Moise Kean, 20, anataka kurudi Juventus, klabu aliyotoka kabla ya kijuiunga na Toffees mwaka 2019. (Calciomercato - in Italian)

Gareth Bale

Rennes imethibitisha kuwa wako kwenye mazungumzo na Chelsea kwa ajili ya Kipa Msenegali, Edouard Mendy, 28. (Goal)

Meneja wa England Gareth Southgate atafanya mazungumzo na kiungo wa Manchester City Phil Foden, 20, na mshambuliaji wa Manchester United Mason Greenwood, 18, baada ya nyota hao kuvunja masharti ya corona wakiwa na timu ya taifa. (Mail)

Bournemouth wanataka kumsainisha kiungo wa pembeni wa Scotland na Newcastle Matt Richie lakini wamekwama kukubaliana na masharti binafsi ya mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 30. (Newcastle Chronicle)

Mlinzi wa kati wa Arsenal na Brazil David Luiz, 33, huenda akaukosa mchezo wa kwanza wa ufunguzi wa msimu huu kufuatia majeraha ya shingo. (Telegraph )

David Luiz

Aston Villa inataka kumsajili mshambuliaji wa Bournemouth na Norway Joshua King, lakini nyota huyo mwenye umri wa miaka 28-anapendelea zaidi kutua Manchester United baada ya uhamisho wake kwenda Old Trafford kukwama kwenye dirisha dogo la usajili la mwezi January. (Athletic - subscription required)

Mshambuliaji wa Arsenal na Ufaransa Alexandre Lacazette, 29, atatafuta ufafanuzi zaidi kuhusu majukumu yake kwenye timu wakati huu tetesi zikisema washika bunduki hao wanataka kumuuza msimu huu. (ESPN)

Aston Villa imeongeza dau zaidi linalovuka £15m kwa ajili ya kumnasa Kipa wa Arsenal Muargentina Emiliano Martinez, 28, baada ya dau lake la kwanza kugonga mwamba. (Goal)

Watford haitamzuia mshambuliaji wake raia wa England Troy Deeney, 32, kutaka kurejea kukipiga Ligi kuu nchini Uingereza. (Mail)

Troy Deeney

Manchester United imekamilisha usajili wa mshambuliaji Alejandro Garnacho,16, kutoka Atletico Madrid. Kinda huyo atawasili kutoka Hipsania baadae wiki hii, na atapaswa kukaa karantini kwa siku 14 days. (Manchester Evening News)

Nottingham Forest wanajiandaa kukamilisha usajili wa beki wa Paris St-Germain na timu ya taifa ya vijana chini ya miaka 21 ya Ufaransa, Loic Mbe Soh, 19. (Goal - in French)

Kiungo wa pembeni wa QPR Bright Osayi-Samuel, 22, anataka Crystal Palace iweke ofa ili kumnasa. (Sky Sports)

TETESI YA JUMATANO

Julian Draxler

Leeds United inajaribu kumshawishi kiungo wa Paris St-Germain na Ujerumani Julian Draxler, 26, ajiunge na klabvu hiyo. (RMC Sport - in French)

Mlinzi wa kati raia England, John Stone 26, anajiandaa kubaki Manchester City msimu huu na kupambania nafasi yake kwenye kikosi cha kwanza cha Pep Guardiola. (Telegraph)

Beki wa Chelsea na England Fikayo Tomori, 22, anakaribia kutua Everton kwa mkopo wa muda mrefu. (ESPN)

Barcelona iko tayari kufufua tena nia yao ya kumsainisha beki wa Kihispania wa Manchester City Eric Garcia, 19. (Mundo Deportivo - in Spanish)

Eric Garcia

Leicester City inaonekana kuizidi kete Manchester United kupata saini ya winga wa Bournemouth na Wales, David Brooks, 23. (Manchester Evening News)

Manchester United wako tayari kusikiliza ofa kwa ajili ya kipa wao Muargentina Sergio Romero, 33, ambapo Aston Villa na Chelsea wanaripotiwa kumtaka. (Express)

United wanafuatilia pia yanayoendelea kuhusu mlinzi wa kushoto Mhispania Sergio Reguilon kwenye klabu yake ya Real Madrid baada ya kuelezwa kwamba nyota huyo mwenye umri wa miaka 23 yuko sokoni, hata hivyo kipaumbele chao cha kwanza ni kuongeza nguvu safu ya ushambuliaji. (ESPN)

Liverpool wanafikiria kumuuza msimu huu mshambuliaji wa timu ya taifa ya chini ya miaka 21, Rhian Brewster, 20, kwa sharti la kumrejesha tena siku za usoni. (Sky Sports)

Rhian Brewster

Arsenal imepewa ofa ya kumsajili kipa wa Ufaransa Alphonse Areola, 27, kwa mkopo wa muda mrefu kutoka Paris St-Germain. (Mirror)

Aston Villa inataka kukamilisha haraka usajili wa kipa Muargentina Emiliano Martinez, 28 kutoka Arsenal, ili awahi kucheza mechi ya ya kufungua msimu jumapili hii. (Mail)

West Brom wanafikiria kumsajili kwa mkopo wa mshambuliaji wa Watford na English,r Andre Gray, 29. (Mail)

Mshambuliaji wa Sheffield United na Jamhuri ya Ireland Callum Robinson anatarajiwa kufanyiwa vipimo vya afya West Brom. Nyota huyo mwenye umri wa miaka 25 anajiandaa kutua kwa uhamisho wa kudumu baada ya kujiunga na timu hiyo kwa mkopo mwezi Januari. (Sky Sports)

Emilio Martinez

West Brom na Leeds zimeongeza nguvu kwenye nia yao ya kumsani kwa mkopo kiungo wa Chelsea na England Conor Gallagher, 20. (Mail)

Bournemouth imepeleka ofa ya kumsajili kwa mkopo beki wa Tottenham na Marekani Cameron Carter-Vickers, 22. (Football Insider)

Bournemouth pia inamtaka kumsajili mshambuliaji wa England Tyrese Campbell, 20, kutoka Stoke City. (Express)

TETESI ZA SOKA JUMANNE

Jadon sancho

Man United inatumai kuwasajili wachezaji watatu kabla ya kukamilika kwa dirisha la uhamisho la msimu huu, huku mshambuliaji wa England na Borussia Dortmund Jadon Sancho 20 akisalia mchezaji wanayemlenga kwa udi na uvumba. (Manchester Evening News)

Uwezo wa mkufunzi wa Real Madrid Zinedine Zidane kukibadilisha kikosi chake kutategemea iwapo Man United itamsajili mshambuliaji wake Gareth Bale. (Marca - in Spanish)

Wawakilishi wa beki wa kushoto wa Porto na raia wa Brazil mwenye umri wa miaka 27 Alex Telles wamesafiri hadi Man United ili kuanza mazungumzo na United. (A Bola, via Metro)

Manchester City imemtambua beki wa Sevilla raia wa Brazil Diego Carlos, 27, na mchezaji wa klabu ya Atletico Madrid na raia wa Uruguay Jose Gimenez, 25, kama mbadala wa beki wa kati wa Napoli na Senegal Kalidou Koulibaly, 29. (Sport - in Spanish)

Diego carlos

Aston Villa inataka kumsaini mchezaji wa England mwenye umri wa miaka 20 Rhian Brewster kutoka Liverpool for £20m. (Sun)

Klabu za ligi ya Premia zinaamini kwamba Brewster ataruhusiwa kuondoka Liverpool katika dirisha hili la mismu wa uhamisho huku klabu za Sheffield United na Crystal Palace pia zikiwa na hamu ya kumsajili mshambuliaji. (Telegraph - subscription required)

Barcelona ina hamu ya kumsajili kiungo wa kati wa Bayern Munich na Uhispania Thiago Alcantara, 29 - ambaye analengwa na Liverpool kurudi katika klabu hiyo. (Bild - in German).

Chelsea inatarajia kukamilisha mkataba na kipa wa Rennes na Senegal Edouard Mendy, 28. (Telegraph)

Thiago Alcantara

The Blues pia wana matumaini ya kuafikia makubaliano na Rennes baada ya kutoa dau la £20m kwa Mendy. (Mail)

Kiungo wa kati wa Chelsea na Ufaransa N'Golo Kante, 29, angekuwa mchezaji anayelengwa na mkufunzi wa Inter Milan Antonio Conte lakini huenda akagharimu £60m. (Calciomercato - in Italian)

West Ham imejiandaa kutoa dau lililoimarika la £30m kumnunua beki wa Burnley na England James Tarkowski, 27. (Evening Standard)

Hatahivyo, Burnley inataka £50m iwapo watalazimika kumuuza mchezaji huyo wa England(Sky Sports)

James Tarkowski

Wolves inakaribia kumsaini kiungo wa kati wa Porto Vitor Ferreira kwa mkopo wa muda mrefu msimu huu huku wakiwa na mbadala wa kumnunua kwa dau £18m. (Express and Star)

Arsenal huenda ikakabidhiwa fursa ya kumsajili beki wa Ghana na Atletico Madrid Thomas Partey, 27, huku klabu hiyo ya Uhispania ikihitaji fedha zaidi za kumnunua kiungo wa kati wa Espanyol na Uhispania Marc Roca 23. (Marca, via Mirror)

Beki wa Spurs na Argentina Juan Foyth analengwa na klabu Villareal. (AS - in Spanish)

Thomas anichzea klabu ya Atletico Madrid ya Uhispania

Chelsea imekataa kumuuza mchezaji wa Ufaransa Tiemou bakayoko kwa dau la chini ya £30m , huku AC Milan ikiwa haitaki kulipa zaidi ya £25m. (Gazetta dello Sport - in Italian)

TETESI ZA JUAMTATU

mshambuliaji wa Barcelona Phillipe Coutinho
Maelezo ya picha,

mshambuliaji wa Barcelona Phillipe Coutinho

Mkufunzi mpya wa Barcelona Ronald Koeman ameambia klabu hiyo anataka kumzuia Phillipe Coutinho msimu huu badala ya kumtoa mchezaji huyo wa Brazil kwa mkopo. (Marca)

Mchezaji wa Scotland Ryan Frazer 12 amekubali kujiunga na klabu ya Newcastle baada ya kuondoka klabu ya Bournemouth mwisho wa msimu na sasa anatarajiwa kufanyiwa vipimo vya matibabu. (Sky Sports)

Mkufunzi wa Manchester United Ole Gunnar Solskjaer amezungumza na winga wa England Jadon Sancho, 20, kuhusu kujiunga na klabu hiyo kutoka klabu ya Borussia Dortmund msimu huu . (Express)

Licha ya Gareth Bale kutaka kuondoka Real Madrid , klabu hiyo haijapokea maombi yoyote ya mshambuliaji huyo wa Wales, huku mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 31 akikataa kupunguziwa mshahara wake na hivyobasi kuwazima wanaommezea mate. (Mundo Deportivo - in Spanish)

Mshambuliaji wa Barcelona Luis Suarez, 33, anatarajiwa kukalia mtihani wa Lugha siku ya Jumatatu ili kupatiwa uraia wa Itali , hatua itakayomfanya kukamilisha uhamisho wake kujiunga na Juventus.(Eurosport)

Mshambuliaji wa Bosnia Edin Dzeko, 34, ameomba kuondoka klabu ya Roma na kujiunga na Juventus. (Corriere dello Sport - in Italian)

Luis Suarez

Barcelona inaandaa ofa ya mwisho kumnunua mshabuliaji wa Argentina Lautaro , 23. (Goal)

West Ham italazimika kuongeza ombi lao la dau la £27m ili kuwa na fursa yoyote ya kumsajili beki wa kati wa Burnley James Tarkowski, 27. (Sun)

Tarkowski anasema kwamba anataka kucheza katika ligi ya mabingwa iwapo fursa itajitokeza na anatumai kurudi katika kikosi cha England. (Telegraph)

Sheffield United inakamilisha dau la £11m kumsaini beki wa Derby na England Jayden Bogle, 20, na Max Lowe, 23, na pia watampeana mshambuliaji wa Ireland Callum Robinson, 25, ili kumpata winga wa Usochi Oliver Burke, 23. (Mail)

James Tarkowski

Mchezaji wa Liverpool na aliyekuwa winga wa timu isiozidi wachezaji wa miaka 21 nchini England Sheyi Ojo, 23, anatarajiwa kujiung na klabu ya Cardiff katika ligi ya daraja la kwanza nchini England kwa mkopo licha ya hamu kutoka Nottingham Forest. (Liverpool Echo)


0 comments:

Post a Comment