Sunday, November 19, 2017

Twitter
Ukiacha North Derby iliyopigwa mchana wa leo, usiku huu kulikuwa na Derby nyingine ya mji wa Madrid ambapo Atletico Madrid wakiwa nyumbani waliikaribisha Real Madrid.
Dakika 90 za mchezo huu zilimalizika kwa Atletico na Real kugawana alama baada ya mchezo huo kutokuwa na mbabe kwa kumalizika kwa sare ya bila kufungana matokeo yanayowafanya wote kubaki na alama 24.
Wakati Derby hiyo ikipigwa pale Hispania, kule nchini Italia kulikuwa na mchezo mkubwa kati ligi ya Serie A ambapo Ac Millan walikwenda kuikabili Napoli.
Milan wameambulia kipigo cha mabao mawili kwa mabao ya Lorenzo Isgne pamona na lile la Piotos Zielinski huku la Millan likiwekwa kimiani na Aressio Romagnoli.
Baada ya mchezo wa leo Sc Napoli wanazidi kujikita kileleni mwa ligi ya Serie A wakiwa na alama 35 huku Ac Millan wakiwa nafasi ya 7 na alama 19.

0 comments:

Post a Comment